Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Kilinisaidia Kujichunguza’

‘Kilinisaidia Kujichunguza’

Kilinisaidia Kujichunguza’

NDIVYO alivyosema msichana mmoja mwenye umri wa miaka 18 aitwaye Maria kutoka jiji la Cherepovets, kuhusu kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Aliandika yafuatayo kwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova karibu na St. Petersburg, Urusi, kilometa 400 hivi kutoka Cherepovets.

“Kichapo hiki kimenisaidia nijichunguze, nichunguze miradi yangu, na watu wanaonizunguka. Nilipata majibu ya maswali ninayopendezwa nayo zaidi. Nilipokuwa nikisoma kitabu hicho, machozi ya shukrani yalinitiririka.”

Maria aliongeza kusema: “Nilihisi kana kwamba nimefumbuliwa macho, ambayo yalifunguka kabisa kwa msisimko. Kitabu hiki ndicho kitabu bora zaidi ambacho nimepata kusoma maishani mwangu. Hakuna kinginecho kinacholingana nacho, kwa kuwa kinategemea Biblia na ushauri wa Yehova Mungu ndio ushauri bora zaidi.”

Ikiwa wewe pia ungependa kunufaika na habari iliyo katika Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, unaweza kupokea nakala yako kwa kujaza na kupeleka kuponi inayoandamana na gazeti hili kwenye anwani iliyoonyeshwa kwenye kuponi au kwenye anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nipelekeeni kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia nyumbani bila malipo.