Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kifaa cha Kufunzia Haki za Kibinadamu

Kifaa cha Kufunzia Haki za Kibinadamu

Kifaa cha Kufunzia Haki za Kibinadamu

MWANAFUNZI aitwaye Rut Jiménez Gila, mwenye umri wa miaka 17 anayeishi huko Granada, Hispania, aliombwa na mwalimu wake aandike insha kuhusu haki za Kibinadamu. Majuma kadhaa baada ya kukamilisha mgawo huo, alifahamishwa na baraza la mitihani la Ulaya lililoko Brussels, Ubelgiji, kwamba alikuwa ameteuliwa pamoja na wanafunzi wengine kadhaa kutoka Hispania ili wawakilishe nchi yao. Baadaye aliwaandikia wachapishaji wa gazeti la Amkeni! barua ifuatayo.

“Nilihitaji habari ya karibuni zaidi kuhusu haki za Kibinadamu, na toleo la ‘Amkeni!’ la Novemba 22, 1998, ‘Je, Haki za Kibinadamu Zitawahi Kupatikana kwa Wote?,’ lilikuwa na habari hususa niliyokuwa nikitafuta. Ili kutoa mifano ya kukiukwa kwa haki za Kibinadamu, niliteua pia habari kutoka kwa makala nyingine za ‘Amkeni!’ juu ya wakati ujao wa wanawake na yale Maangamizi Makubwa. [Ona toleo la Aprili 8, 1998, na Agosti 8, 1998.] Katika utafiti wangu niligundua kwamba ‘Amkeni!’ lilikuwa na habari ambazo singeweza kuzipata katika magazeti mengine au vitabu vya marejezo. Nilivutiwa pia na picha, na nilitia baadhi yake katika ripoti yangu.

“Kwa sababu ya insha yangu iliyoshinda tuzo, nilikaa Finland kwa muda wa juma moja, na huko niliweza kuzungumza zaidi juu ya haki za Kibinadamu na kueleza thamani ya gazeti la Amkeni! katika kukazia masuala muhimu kama hilo.

“Asanteni sana, kwa sababu ya kuwa wa kwanza sikuzote kutujulisha matukio ya ulimwengu. Yehova na aendelee kuwabariki, ili mamilioni ya watu waendelee kunufaishwa na habari hiyo.”

[Picha katika ukurasa wa 15]

Rut akiwa na cheti cha kushiriki alichotuzwa