Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Siku ya Kukumbukwa

Siku ya Kukumbukwa

Aprili 19, 2000

Siku ya Kukumbukwa

JIONI ya kabla ya kufa kwake, Yesu alianzisha ukumbusho wa kifo chake. Ilikuwa sherehe sahili. Wakati huo aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Fulizeni kufanya hili katika ukumbuko wangu.”—Luka 22:19.

Mwaka huu ukumbusho wa tukio hilo utakuwa Jumatano, Aprili 19, baada ya jua kutua.

Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote watakusanyika jioni hiyo ya pekee ili kuadhimisha Ukumbusho huu namna Yesu alivyoomba ufanywe. Unaalikwa kwa uchangamfu sana ujiunge nao mkiwa watazamaji. Tafadhali uliza Mashahidi wa Yehova saa hasa na mahali pa kukutana.