Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kitabu Chenye Mwongozo Halisi na Chenye Kutumika”

“Kitabu Chenye Mwongozo Halisi na Chenye Kutumika”

“Kitabu Chenye Mwongozo Halisi na Chenye Kutumika”

KATIKA majira ya kiangazi yaliyopita gazeti la Arkansas Democrat Gazette lilipitia vitabu kadhaa vilivyochapishwa na Watch Tower Bible and Tract Society. Kuhusu mojawapo ya vitabu hivyo, lilitaarifu hivi: “Maswali Ambayo Vijana Huuliza ni kitabu chenye mwongozo halisi na chenye kutumika kwa familia zote, bila kujali dini yao. . . .

“Kitabu hiki huwaandalia wasomaji wake mashauri mengi yanayofaa kiadili na kihisia-moyo. Kwa mfano, waandikaji wake wanafahamu kwamba vijana wote hutaka kuwa huru kutokana na vizuizi vya wazazi, lakini kinawapa vijana shauri lifuatalo:

“‘Je, wataka uhuru na madaraka zaidi? Basi jithibitishe kuwa mwenye kuchukua madaraka kwa uzito. Chukua kwa uzito kazi zozote unazogawiwa na wazazi wako.’

“Wazazi wengi huthamini kitabu kinachokazia sana uwajibikaji na kuwaonya sana vijana kwa upole wajiheshimu na kuwaheshimu wengine. Ingawa sikuzote kitabu hicho hutegemeza shauri lake kwa Biblia, kinategemea sana hekima inayotumika na utambuzi. . . . Sehemu inayozungumzia kujistahi ni yenye kuvutia sana, kwa kuwa vijana wengi wamekosea kwa kufikiri kwamba ni vizuri kujiona kupita kiasi.”

Baada ya kunukuu kitabu hicho, makala hiyo iliendelea kusema: “Kikumbusha hiki cha upole kwamba kujivuna ni kiburi na kwamba unyenyekevu ni msingi wa maisha ya Kikristo ni bora kuliko baadhi ya mashauri ya kipuuzi yanayopendwa ya saikolojia ambayo vijana hupata kutoka kwa marafiki na washauri wenye nia nzuri.”

Ikiwa wapenda kunufaika kutokana na habari iliyomo katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, waweza kupokea nakala kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia nyumbani bila malipo.