Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi ya Kufurahia Maisha ya Familia

Jinsi ya Kufurahia Maisha ya Familia

Jinsi ya Kufurahia Maisha ya Familia

“NIMEKUWA nikisoma gazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa miaka 40,” aandika Graciela kutoka Argentina, Amerika Kusini. “Leo, baada ya miaka mingi sana, naweza kusema kwamba yametimiza mahitaji yangu. Yalinisaidia utotoni, nilipokuwa tineja, wakati wa uchumba na ndoa, na katika kuwalea watoto wangu sita.

“Magazeti hayo hunisaidia pamoja na mume wangu kulea watoto wetu wanne ambao bado wanaishi nyumbani. Nayatumia ifaavyo magazeti hayo kuzungumza na watoto wangu na walimu wao shuleni. Nilisoma Amkeni! moja kwa moja nilipokuwa nikizungumza na madaktari kuhusu matatizo ya afya. Kwa msaada wa mfululizo wa makala wenye kichwa “Msaada kwa Watoto Wenye Kasoro za Kujifunza” (Februari 22, 1997), tuligundua kwamba mmoja wa binti zetu ana tatizo la kujifunza.”

Vichapo vya Watch Tower Society vyaweza kusaidia familia zikabili matatizo mengi yanayowakumba na kufurahia maisha pamoja. Kwa mfano, kitabu chenye kurasa 192 Siri ya Kupata Furaha ya Familia chaweza kunufaisha waume, wake, wazazi, watoto, babu na nyanya—naam, kila mshiriki wa familia. Zifuatazo ni baadhi ya sura zake zenye kuelimisha: “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana,” “Saidia Tineja Wako Asitawi,” “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” na “Unaweza Kushinda Matatizo Yanayoidhuru Familia.”

Ili upate nakala, tafadhali jaza na kutuma kuponi iliyo hapa, kwa kutumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili. Utapokea madokezo hususa yanayoweza kukusaidia kutatua matatizo na kufanya maisha ya familia yapendeze kama alivyokusudia Muumba.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Graciela na familia yake