Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Nilifikiri Daima Kuwa Ni Mimi Tu”

“Nilifikiri Daima Kuwa Ni Mimi Tu”

“Nilifikiri Daima Kuwa Ni Mimi Tu”

MANENO hayo yalisemwa na Ulrike, msichana wa miaka 13 kutoka huko California, Marekani, baada ya kusoma kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Aliandika hivi:

“Nilifurahi kuona katika kitabu hicho ile sura ‘Familia za Mzazi Mmoja Zaweza Kufanikiwa!’ Ilinisaidia kumtendea mama yangu kwa fadhili na kumsaidia zaidi kwa sababu yeye ni mzazi mmoja. Ilinisaidia pia kuelewa zaidi hisia zake. Nilifikiri daima kuwa ni mimi tu niliyekuwa nikiumia kihisia.” Kijana huyo alimalizia kwa kusema: “Kitabu hicho kilinisaidia sana!”

Kitabu hiki chenye kurasa 192 kimenufaisha mamilioni ya watu ulimwenguni pote. Kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia chaweza kunufaisha washiriki wote wa familia—waume, wake, wazazi, watoto, babu, nyanya—naam, kila mtu. Baadhi ya sura zake zenye kuelimisha ni “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana,” “Saidia Tineja Wako Asitawi,” “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” na “Dumisha Amani Nyumbani Mwako.”

Ili upate nakala yako, tafadhali jaza kuponi iliyopo hapa na uitume kwenye anwani iliyoonyeshwa au kwenye anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili. Utapokea madokezo hususa yanayoweza kukusaidia kutatua matatizo na kufanya maisha ya familia yapendeze kama Muumba alivyokusudia.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia nyumbani bila malipo.