Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Mnawaonyesha Watu Wote Upendo’

‘Mnawaonyesha Watu Wote Upendo’

‘Mnawaonyesha Watu Wote Upendo’

MANENO hayo ya pongezi yaliandikiwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Yugoslavia, nchi ambamo watu wa makabila mbalimbali wamekuwa wakipigana kwa karne nyingi. Barua hiyo ilisema hivi:

“Mabwana,

Nimesikia habari nyingi kuwahusu nyinyi Mashahidi wa Yehova katika mji wangu wa nyumbani wa Sarajevo, lakini sikuwahi kupendezwa kamwe na itikadi zenu hadi nilipopata fursa ya kuhudhuria mkusanyiko wenu huko Ujerumani kiangazi kilichopita. Nilivutiwa sana kuona watu kutoka Kroatia, Yugoslavia, na Bosnia wakiwa wameketi pamoja kwa amani na hata wakiitana ndugu na dada. Sikuwahi kuona jambo kama hilo! Upendo mlio nao ni ithibati yenye nguvu kwamba siasa haziwezi kuwagawanya. Mungu na awabariki kwa sababu ya upendo mnaoonyesha watu wote!”

Ripoti kama hizo kutoka maeneo yenye uhasama wa muda mrefu hutokeza swali hili, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Swali hilo ni kichwa kikuu cha broshua yenye kurasa 32 yenye kutoa ushuhuda wenye nguvu juu ya uwezekano wa kuwako kwa ulimwengu wa aina hiyo. Jinsi gani? Na lini?

Waweza kupokea nakala ya broshua hii kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa kwenye kuponi au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.