Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Dunia—makao ya Milele ya Viumbe

Dunia—makao ya Milele ya Viumbe

Duniamakao ya Milele ya Viumbe

VIUMBE chungu nzima walio duniani hutukumbusha maneno ya Zaburi 104:24, 25: “Ee, BWANA, jinsi yalivyo mengi matendo yako! Kwa hekima umevifanya vyote pia. Dunia imejaa mali zako. Bahari iko kule, kubwa na upana, ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika, viumbe hai vidogo kwa vikubwa”—na twaweza kuongezea, hata katika sehemu zisizokalika!

Hata hivyo, inasikitisha kwamba kutojua kwa mwanadamu na pupa yake kumesababisha viumbe fulani kutoweka kabisa na wengine wamo hatarini. Tatizo moja kuu ni uchafuzi. Ndiyo sababu baadhi ya wanasayansi wanachunguza viumbe fulani hususa wanaostahimili sumu na joto kali—kama wale wanaoishi karibu na matundu yaliyo katika vilindi vya bahari na katika chemchemi za maji moto kama zile zilizo katika Mbuga ya Taifa ya Yellowstone—kwa lengo la kuiga mbinu zao za pekee za kuondoa vichafuzi. Wakati huohuo, wanasayansi wengine wanajaribu kuelewa kikamili zaidi mifumo inayotegemeza uhai duniani inavyofanya kazi na jinsi ambavyo wanadamu hutenda katika mifumo hiyo.

Mfumo wa Majaribio wa Kutegemeza Uhai

Ili kuweza kuelewa vyema zaidi mifumo ya kutegemeza uhai duniani, wanasayansi walifanya majaribio katika miaka ya 1990 kwa kutumia mfumo uliofunikwa kabisa huko Arizona, Marekani. Waliuita Biosphere 2 (dunia ikiwa “Biosphere 1”) kwa sababu walitarajia kwamba ungetegemeza uhai pasipo msaada. Ulikuwa na zaidi ya jamii 3,000 za viumbe, pamoja na wanadamu wanane. Viumbe wote walitengwa humo mbali na mazingira ya dunia kwa muda wa miaka miwili. Lakini, matatizo makubwa yalizuka kwenye Biosphere 2. “Karibu ndege wote, wanyama na wadudu waliotarajiwa kusitawi humo walikufa—isipokuwa mende na ‘siafu wenye kichaa,’” ikasema ripoti moja, na kuongezea kuwa “mradi mzuri wa Biosphere 2 ukawa kitu cha kufedhehesha.” Majaribio hayo yasiyofua dafu yalithibitisha kwa njia kubwa kama nini akili iliyotumiwa kubuni “Biosphere 1”!

Muumba Ndiye Atakayeokoa Dunia!

Kadiri tunavyojifunza mengi kuhusu dunia na viumbe wake wa kustaajabisha, ndivyo tunavyopaswa kusitawisha heshima kubwa kuelekea sayari hii yenye uwezo kwelikweli na Muumba wake mwenye hekima isiyo na kikomo. Bila shaka, watu wengi huonyesha kwamba wanaipenda dunia, labda kwa kujihusisha mno na masuala ya mazingira. Lakini jambo la kusikitisha ni kwamba watu hao hukabili vizuizi wasivyoweza kushinda, kama vile pupa ya mwanadamu na kutojua, mambo ambayo hayawezi kukomeshwa hata na watu wenye nia nzuri kabisa.

Hata hivyo, watu wanaohangaikia tatizo hilo kwa unyofu wanaweza kufarijiwa na ahadi ya Biblia ya kwamba hivi karibuni Mungu mwenyewe ataangamiza watu wote wenye pupa, wasiomhofu yeye ambao ‘wanaiangamiza dunia.’ (Ufunuo 11:18; 2 Timotheo 3:1-5) Baadaye, Muumba, ambaye jina lake ni Yehova, ataanzisha programu ya kurekebisha mambo upya, ambayo itasafisha kabisa dunia na kuigeuza kuwa chemchemi ya uhai ya kiparadiso.—Zaburi 83:18; Isaya 35:1, 2.

Usafishaji huo utatimizwa kupitia kwa Ufalme wa Mungu—serikali ya kimbingu mikononi mwa Kristo Yesu. (Danieli 2:44; Mathayo 6:9, 10) Chini ya utawala wake, Dunia sayari itasitawi, kwa kuwa itatunzwa na wanadamu wanaomhofu Mungu ambao wanapendezwa na enzi kuu ya Yehova na wanastahi sana kazi zake. (Zaburi 37:10, 11; Ufunuo 21:3, 4) Kwa nini twaweza kuwa na hakika kwamba ahadi hizo zitatimizwa? Kwa sababu “sifa [za Mungu] zisizoonekana,” kama zifunuliwavyo katika uumbaji na katika Biblia, huthibitisha kwamba “kwa Mungu hakuna tangazo lolote litakalokuwa lisilowezekana.”—Waroma 1:20; Luka 1:37.

[Picha katika ukurasa wa 12]

Hivi karibuni dunia yetu itakuwa paradiso