Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Tulikusudiwa Kuishi Milele”

“Tulikusudiwa Kuishi Milele”

“Tulikusudiwa Kuishi Milele”

Hiyo ilikuwa kauli ya mwanamume mmoja kutoka Kasama, Zambia, kuhusu kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Aliandika hivi kuhusu Muumba wetu:

“Nilipata kumfahamu Yehova kwa njia mpya kabisa baada ya kumaliza kusoma kitabu hicho. Nilivutwa kwake hata zaidi baada ya kusoma jinsi ambavyo miili yetu imeumbwa kwa ustadi. Hakuna shaka yoyote kwamba tulikusudiwa kuishi milele.”

Ushuhuda wa mambo hayo unazungumziwa katika sura ya 4, yenye kichwa “Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!” ambapo mbali na habari kuhusu umbo la ubongo, mambo kama lugha, hekima, na utu wa mwanadamu yanazungumziwa pia.

Twakukaribisha uchunguze uthibitisho wa sayansi na uone kama hutakubaliana na kauli ya kitabu hiki: “Kadiri tujifunzavyo kuhusu utendaji wa ubongo wetu na akili zetu, ndivyo iwavyo rahisi kuona ni kwa nini mamilioni ya watu wamekata kauli ya kwamba hali ya mwanadamu ya kufahamu kuwako kwake ni uthibitisho wa kuwako kwa Muumba ambaye anatujali.”

Waweza kupokea nakala ya kitabu hiki chenye kurasa 192 kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

J. Hester and P. Scowen (AZ State Univ.), NASA