Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mwenye Shaka Lakini Bado Anatafuta

Mwenye Shaka Lakini Bado Anatafuta

Mwenye Shaka Lakini Bado Anatafuta

KATIKA barua kwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Slovenia, mwanamume aliyedai kuwa Mkatoliki aliyebatizwa alisema hivi: “Tafadhali nitumieni nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Pia ningependa kujua namna niwezavyo kupokea kwa ukawaida gazeti la Amkeni! hapa nyumbani.”

Mwanamume huyo alieleza hivi: “Tafadhali msinielewe vibaya. Mimi hutilia shaka dini, lakini nilishangaa sana niliposoma Amkeni! kwa kuwa haliwalazimishi wasomaji wake wafuate kauli zake bali lilieleza mambo kinagaubaga na kwa njia yenye kufundisha.” Kisha akarejezea gazeti moja mashuhuri la kidini na kusema kwamba linawalazimisha watu wafuate kauli zake.

Mwanamume huyo alieleza sababu yake ya kutojaza kuponi inayopatikana ukurasa wa nyuma wa Amkeni! ili kuomba broshua Anataka na badala yake akachagua kuandika barua mwenyewe. “Sikutaka kuharibu gazeti hilo la Amkeni!,” akasema. “Nilitaka kulihifadhi lote!”

Broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? yenye kurasa 32 ina masomo 16. Masomo hayo yana mafundisho ya msingi ya Biblia na habari kutoka kwa Biblia inayoonyesha yale tunayopaswa kufanya ili kupata kibali cha Mungu. Ikiwa ungependa pia kupokea nakala ya broshua hii, jaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Nakala milioni 113 katika lugha 240