Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Shauri la Wakati Ufaao’ Kwa Kila Mtu

‘Shauri la Wakati Ufaao’ Kwa Kila Mtu

‘Shauri la Wakati Ufaao’ Kwa Kila Mtu

“NILIGUSWA sana hadi nikatokwa na machozi na hilo ‘shauri madhubuti’ na la wakati ufaao,” akaandika msomaji mmoja wa kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. “Nimeguswa sana na jinsi kitabu hicho kinavyoshughulikia (kupitia kanuni) kila aina ya magumu yawezayo kutokea katika familia. . . . Nimesoma hadi katikati ya sura ya 8 ya kitabu hicho na nikaamua kuwaandikia. Singeweza kusubiri zaidi.”

Msomaji huyo mwenye kuthamini kutoka North Carolina, Marekani, aliongeza kusema: “Nasali kwamba washiriki wa familia yangu na watu wengine wengi duniani pote, watasoma kwa uangalifu yaliyomo ndani ya kitabu hicho.”

Mamilioni ya watu kote duniani wamenufaishwa na kitabu hiki cha kurasa 192. Kitabu hicho chaweza kunufaisha washiriki wote wa familia—mume, mke, wazazi, watoto, babu na nyanya. Baadhi ya sura zake zenye kuelimisha ni “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana,” “Saidia Tineja Wako Asitawi,” “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” na “Dumisha Amani Nyumbani Mwako.”

Waweza kupokea nakala yako kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili. Utapokea madokezo hususa yanayoweza kukusaidia kutatua matatizo na kuyafanya maisha ya familia yawe yenye kupendeza kama Muumba alivyokusudia.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.