Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Kweli Mungu Yuko?

Je, Kweli Mungu Yuko?

Je, Kweli Mungu Yuko?

Nchini Thailand, mwanamume mmoja kijana alisema kwamba alikuwa ameomba Mungu hivi: “Mungu, ikiwa kwa kweli wewe uko, nisaidie kujifunza njia zako.” Baadaye, mwanamume huyo alieleza hivi:

“Mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuja nyumbani kwangu, lakini sikuwako. Aliacha trakti na kikaratasi cha mwaliko kilichokuwa na ramani ya mahali pa mikutano.” Mwanamume huyo alifuata mwelekezo wa kikaratasi hicho. Alisema hivi: “Jumba lilikuwa safi sana na la kawaida tu, na watu walikuwa wachangamfu na wenye urafiki.

“Jambo jingine lililonivutia lilikuwa kwamba kila mtu alikuwa na Biblia yake mwenyewe na aliifungua na kuisoma msemaji aliposoma maandiko. Hivyo ndivyo nilivyohisi mtu anapaswa kujifunza Biblia ili ajue kiini cha mafundisho ya kweli ya kidini. Nilishangaa pia kuona watoto wakishiriki funzo na kutoa maelezo pia. Sikuwa nimeona jambo kama hilo hapo awali.”

Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? ni mojawapo ya vichapo vya Biblia vinavyotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika mikutano yao. Waweza kupokea kitabu hicho chenye kurasa 192 na kilichojadiliwa kwa karatasi, kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

“Nguzo za Uumbaji” kwenye jalada la kitabu: J. Hester and P. Scowen (AZ State Univ.), NASA