Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Si kwa Vijana Tu

Si kwa Vijana Tu

Si kwa Vijana Tu

Katika barua yake kwa ofisi ya usimamizi ya Mashahidi wa Yehova huko Poland, Jolanta, aliye na umri wa miaka 25, alieleza kwamba alikuwa ameshuka moyo. Yeye ni mlemavu asiyeweza kutembea, na mama yake na nyanya yake wote walikufa katika kipindi cha miezi sita. Lakini alianza kusoma kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Aliandika hivi:

“Nilifikiri kwamba kitabu hicho kinafaa vijana wala si mimi,” aliandika. “Nilikosea kama nini! Nilipojifunza sura 12 hadi 16 katika kitabu hicho, nilipata majibu kwa maswali yangu: ‘Kwa nini ninashuka moyo sana na kujihisi mpweke?’ ‘Kwa nini sijipendi?’ na ‘Kwa nini nimehuzunika sana baada ya [vifo vya] wapendwa wangu?’”

Aliongeza kusema hivi: “Hoja mbili kwenye ukurasa wa 130 zilinivutia: ‘Kujua kwamba kihoro chako ni jambo la kawaida ni msaada mkubwa katika kukabiliana nacho. Lakini kule kuendelea kukana ukweli wa mambo hurefusha muda wa kihoro tu.’ Kusoma maneno hayo kuliimarisha tumaini langu la kuona tena wale waliokufa, na kulifanya maisha yangu yawe na kusudi zaidi.”

Ukitaka kushinda hisia za kushuka moyo na kuwa na kusudi maishani, tunahisi kwamba utafaidika kwa kusoma kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Waweza kupokea nakala kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza —Majibu Yafanyayo Kazi. Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.