Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ugumu wa Kuwatunza Watoto

Ugumu wa Kuwatunza Watoto

Ugumu wa Kuwatunza Watoto

Uingereza ni nchi ya Magharibi yenye ufanisi. Hata hivyo, yakadiriwa kwamba kila mwaka zaidi ya watoto 100,000 nchini humo—mara mbili zaidi ya ilivyokuwa imekadiriwa—hutoroka nyumbani. Matokeo ni kwamba mtoto 1 kati ya watoto 7 huumia kutokana na ujeuri au kubakwa.

“Watoto wanapohisi wamepuuzwa na kwamba hawapendwi, waweza kufikiri kwamba kutoroka ndio suluhisho,” asema Ian Sparks, mkurugenzi mkuu wa Shirika la Watoto. Aongezea hivi: “Jambo hilo huwapata watoto wa tabaka zote—watoto wanaoishi kwenye nyumba za matajiri hutoroka kama tu wale wanaoishi katika nyumba za jijini za bei nafuu.”

Ni daraka zito kuwatunza na kuwazoeza watoto. Msaada waweza kupatikana wapi? Kichapo Siri ya Kupata Furaha ya Familia kimeandikwa ili kuandaa msaada huo. Baadhi ya sura zake 16 ni: “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana,” “Saidia Tineja Wako Asitawi,” na “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu.” Sura zote 16 za kitabu hicho zina mashauri yenye kutumika na, la maana zaidi, zinategemea Biblia kama chanzo cha hekima inayozidi hekima yetu.

Waweza kuomba nakala ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kwa kujaza kuponi iliyo hapa na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Onyesha lugha unayotaka.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.