Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Sijasoma Kamwe Kitabu Kama Hiki”

“Sijasoma Kamwe Kitabu Kama Hiki”

“Sijasoma Kamwe Kitabu Kama Hiki”

Kijana aitwaye Łukasz anayeishi karibu na Szczecinek kaskazini mwa Poland alivutiwa sana na kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Aliamua kwenda nacho shuleni na kumpa mwalimu wake wa fizikia. Alielekeza fikira zake kwenye habari kuhusu ulimwengu. Akamwonyesha picha kwenye ukurasa wa 78 (inayoonyeshwa hapa). Kitabu hicho kinaonyesha dhana mbalimbali kuhusu mwanzo wa ulimwengu, ambazo wewe pia unaweza kutafakari.

Baadaye mwalimu huyo alimwambia Łukasz hivi: “Sijasoma kamwe kitabu kama hiki. Mambo tata ya kisayansi yameelezwa kifupi na kwa njia rahisi yenye kueleweka! Ikiwa ningalipata kitabu hicho mapema, singalinunua kitabu kipya cha masomo cha fizikia kwa ajili ya shule ya sekondari. Kwa hakika nitatumia kitabu hicho darasani.”

Baada ya kusoma kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? watu wengi wametiwa moyo kutafakari zaidi chanzo na kusudi la maisha na vilevile jinsi sisi tulivyopata kuwapo. Na jambo la maana hata zaidi ni kwamba kitabu hicho kimewasaidia wengi kufikia uamuzi mzuri.

Wewe pia unaweza kuomba nakala ya kitabu hiki chenye kurasa 192 kwa kujaza kuponi iliyopo hapa na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Onyesha lugha unayotaka.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Courtesy of Anglo-Australian Observatory, photograph by David Malin

“Nguzo za Uumbaji” kwenye jalada la kitabu: J. Hester and P. Scowen (AZ State Univ.), NASA