Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Hekaheka Ule mfululizo, “Kukabiliana na Hekaheka za Leo” (Februari 8, 2001) ulizungumzia kiini cha matatizo ya jamii yetu ya kisasa. Swali, “Je, wewe unatanguliza watu au mali?” lilinivutia sana. Tafadhali endeleeni kuchapisha makala hizo zenye kupendeza!

Y. K., Japani

Makala hizo zilinisaidia kutambua mambo ya kutanguliza na namna ya kuchanganua shughuli zangu. Bila kujua, maisha yangu yalinifanya nijihisi mchovu daima, nihangaike na kuchoka kiakili. Sasa ninabadili mazoea yangu na kutanguliza mambo yaliyo muhimu. Asanteni kwa kunisaidia kufanya maisha yangu kuwa sahili!

L.D.C., Guatemala

Mfumo wa Kinga Nilimpa daktari mmoja anayehusika na madawa ya kinga, toleo la Februari 8, 2001, lililokuwa na makala “Walinzi Wanaolinda Afya Yako.” Alifurahia picha iliyo kwenye ukurasa wa 15 iliyoonyesha chembe nyeupe za damu zikishambulia bakteria. Aliikuza picha hiyo na kuiweka katika fremu, na sasa anaitumia kuwafundisha wengine kuhusu mfumo wa kinga.

H. K., Japani

Nimekuwa nikisoma gazeti la Amkeni! kwa miaka 30, nami nathamini sana ujumbe wake wa wakati unaofaa. Nilipendezwa hasa na makala ya “Walinzi Wanaolinda Afya Yako” kwani ilinisaidia kuelewa namna mfumo wa kinga tuliopewa na Yehova unavyofanya kazi kwa njia ya ajabu.

L. G., Mexico

Mimi ni daktari, na nilijifunza elimu ya kingamaradhi nilipokuwa mwanafunzi wa tiba. Maelezo ya kitabu cha mafunzo kuhusu mfumo wa kinga yalikuwa magumu kueleweka, lakini makala hiyo ilikuwa yenye kupendeza sana. Ilitoa muhtasari kwa njia yenye kueleweka. Wakati mmoja mhadhiri alisema kwamba tunapojifunza kuhusu mfumo wa kinga hatuwezi kupuuza wazo la kwamba uliumbwa na Mungu. Natazamia makala nyingine zenye kupendeza kuhusu mwili wa binadamu.

N. K., Japani

Tsunami Nina umri wa miaka 12, nami husoma magazeti yenu yote. Nilipendezwa sana na makala, “Mawimbi Yanayofisha—Hekaya na Ukweli.” (Februari 8, 2001) Mawimbi hayo hunivutia sana na nilifurahia namna mlivyoeleza kwa njia ya mfano jinsi yalivyo yenye nguvu.

K. S., Marekani

Cheche za Mnururisho Nilivutiwa sana na yale maelezo yenye kueleweka katika makala “Cheche za Mnururisho —Suala Linalohangaisha.” (Februari 22, 2001) Nilijua kwamba elementi kama strontium 90 ni zenye madhara sana, lakini sikujua kwamba zinaathiri mwanadamu tangu utotoni. Kuelewa habari zilizo tata jinsi hii kunawasaidia watu kutambua kwamba ili kupata suluhisho, mwanadamu anahitaji msaada wa Muumba Mtukufu. Asanteni sana kwa hangaiko mnalozidi kuwaonyesha wasomaji wenu kwa kurahisisha habari hizi ngumu ili kila mtu anufaike nazo.

M. Z., Italia

Vijana Huuliza Nimekuwa nikisoma gazeti la Amkeni! tangu lilipokuwa linaitwa Consolation. Nijapokuwa mzee, nafurahia kusoma makala za “Vijana Huuliza . . . ” Kwa kutumia baadhi ya habari hizo maishani mwangu, nimepata ujuzi na mashauri mazuri zaidi. Mfululizo huu unaelimisha hata wazee kama mimi.

R. S., Marekani