Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu Yaweza Kupatikana Wapi?

Majibu Yaweza Kupatikana Wapi?

Majibu Yaweza Kupatikana Wapi?

Watu wengi huuliza swali hilo siku hizi. Mwalimu mmoja huko Novosibirsk, Urusi, alisema kwamba si rahisi kupata majibu kwa maswali ambayo wanafunzi wake huuliza kuhusu Mungu na dini. Aliandika hivi katika barua:

“Siku moja nilipofika nyumbani, nilipata trakti iliyokuwa imeachwa hapo yenye kichwa ‘Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia.’ Mimi hufundisha historia shuleni, na mara nyingi ninalazimika kuzungumza na wanafunzi kuhusu dini, Biblia, na Mungu. Nyakati nyingine, inakuwa vigumu kuwajibu watoto.

“Zamani, nilidhani watu husali kwa Mungu wanapokuwa na shida tu. Lakini sasa nina uhakika kwamba jambo hilo si kweli. Pia, mtu huuliza hivi: ‘Kwa nini jambo hilo limenipata? Mimi ni nani? Nilitoka wapi? Nitaenda wapi nikifa?’ Ni jambo la maana kupata majibu kwa maswali hayo. Yaonekana Biblia hutoa sababu zinazosadikisha.”

Mwalimu huyo alimalizia hivi: “Niliandika barua hii kwa kuwa ninataka kujua mengi zaidi kuhusu Biblia na Mungu.”

Mashahidi wa Yehova huwaelekeza watu kwenye Biblia ili wapate majibu kwa maswali yao. Fikiria kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kati ya sura zake 19 kuna zile zenye vichwa hivi: “Mungu wa Kweli Ni Nani?,” “Sababu Gani Tunazeeka na Kufa?,” na “Sababu Gani Mungu Huruhusu Kuteseka?” Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho cha kujifunzia Biblia chenye kurasa 192 kwa kujaza na kutuma kuponi iliyo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Onyesha lugha unayotaka.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.