Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Chuki Ndugu yangu alikuja kunitembelea hivi majuzi. Sikujua kwamba yeye ni mtu wa kushikilia sana maoni yake. Alizungumza kuhusu watu wa rangi tofauti kwa ukali na kwa dharau. Nilitaka kumsaidia lakini sikujua jinsi ya kufanya hivyo. Nilipoliona toleo la Amkeni! la Agosti 8, 2001, lenye mfululizo “Kukomesha Chuki,” nilijua mara moja kwamba sala yangu imejibiwa.

L. B., Marekani

Mtu mwenye akili hawezi kukubaliana nanyi juu ya taarifa hii mliyotoa: “Biblia yenyewe yasema kwamba wanadamu wasiokamilika wamezaliwa wakiwa na tabia mbaya na kasoro. (Mwanzo 6:5; Kumbukumbu la Torati 32:5) Kwa wazi, maneno hayo yanawahusu wanadamu wote.” Maandiko hayo yanazungumzia vikundi viwili vya watu walioishi katika vipindi mbalimbali vya wakati na mahali tofauti. Hayahusu wanadamu wote hata kidogo.

D. C., Jamhuri ya Cheki

“Amkeni!” linajibu: Ni kweli kwamba maneno hayo yalihusu Waisraeli na watu walioishi kabla ya Gharika. Hata hivyo, Biblia inaonyesha wazi kwamba “wote wamefanya dhambi na hupungukiwa na utukufu wa Mungu.” (Waroma 3:23; 5:12; Ayubu 14:4; Zaburi 51:5) Kwa hiyo, Waisraeli na watu walioishi kabla ya Gharika walitajwa ili kuonyesha kutokamilika kwa wanadamu.

Vitabu vya Kumbukumbu Nilifurahia sana kusoma makala ya “Kitabu cha Kumbukumbu—Rafiki Anayetumainika.” (Agosti 8, 2001) Nina umri wa miaka 20 na nimeandika kitabu cha kumbukumbu tangu nilipokuwa na umri wa miaka 11. Ninafurahia sana kusoma juu ya mizaha yangu, wavulana niliowapenda zamani, mashairi yangu, jinsi nilivyojiaibisha, na hata kuhusu ubatizo wangu na jinsi nilivyohisi siku hiyo.

L. C., Italia

Nilitendwa vibaya nilipokuwa mtoto. Kuandika kitabu cha kumbukumbu kumenisaidia kujijua vizuri zaidi na kupunguza uchungu wa moyoni. Nimefanya maendeleo ya kiroho.

E. L., Marekani

Ugonjwa wa Mfumo wa Kinga Jana nilifanyiwa upasuaji wa dharura, na yaelekea jicho langu la kushoto litapofuka. Nilishtuka sana na kushuka moyo. Nilipofika nyumbani nilipata toleo la Amkeni! la Agosti 8, 2001, lenye simulizi la Marc Holland lenye kichwa “Pambano Langu na Ugonjwa wa Mfumo wa Kinga.” Nilitiwa moyo sana kuona jinsi alivyovumilia ugonjwa huo mbaya, hasa imani yake na azimio lake la kuendelea kumtumikia Yehova. Nilipolinganisha hali yangu na yake, tatizo langu lilionekana kuwa dogo sana.

L. B., Marekani

Sala Asanteni kwa makala ya “Vijana Huuliza . . . Sala Yaweza Kunisaidiaje?” (Julai 22, 2001) Ninaposoma jinsi ambavyo vijana wengi wamesaidiwa kushinda matatizo yao kwa kutoa sala ninatiwa moyo kusali kwa Yehova kutoka moyoni.

D. B., Italia

Makala hiyo ilinisaidia kutambua kwamba ninahitaji kumkaribia Mungu zaidi. Ni vigumu sana kwa kijana mwenye umri wa miaka 16 kufanya hivyo. Kuna vishawishi vingi, na uvutano mwingi wa marafiki. Ninaweza kupata Biblia jinsi gani?

M. A., Marekani

“Amkeni!” linajibu: Mipango ilifanywa ili Mashahidi wa Yehova wamtembelee msomaji wetu na kumpa Biblia.

Nilipenda maneno ya kijana Paul, aliyesema kwamba alimwomba Yehova ampe amani ya akili. Sikuzote maishani mwangu nimemwomba Yehova anisaidie kuwa thabiti akilini na moyoni, na kufanya maamuzi kwa busara. Sasa nitamwomba anipe amani ya akili pia. Tunaweza kujifunza mengi kutoka kwa vijana. Nina umri wa miaka 62.

M. P., Australia