Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Mfadhaiko wa Tukio Lenye Kutisha Nilipopokea toleo la Agosti 22, 2001 la Amkeni! lenye kichwa “Kupambana na Mfadhaiko wa Tukio Lenye Kutisha,” nilishangaa sana hivi kwamba nililia sana. Nimekuwa nikimwomba Yehova kwa muda mrefu anionyeshe jinsi ya kukabiliana na mfadhaiko wangu. Nilidhani kwamba sikuwa na thamani yoyote na nilianza kuhisi sifai kitu. Leo sala zangu zilijibiwa. Makala hizo zimenifaidi sana kiroho na kihisia.

C. K., Japani

Nina umri wa miaka 40 na ninafadhaishwa na mambo yaliyonipata utotoni. Makala zenu zilijibu sala zangu. Zilikuwa zenye kutia moyo na zenye kujenga. Asanteni kwa makala hizo zenye ufikirio. Endeleeni kuzichapisha!

R.D.M., Marekani

Si rahisi kueleza uchungu wa kuishi na mfadhaiko wa tukio lenye kutisha. Baba yangu alikuwa mraibu wa kileo, na tangu utoto wangu niliishi na hasira yake na ujeuri wake. Pia, nilitendwa vibaya kingono. Nilifurahi kwa sababu makala hizo zilitaja kuwa wale wanaougua mfadhaiko wa tukio lenye kutisha huelekea kujilaumu na hivyo wanahitaji sana kitia-moyo. Namshukuru Yehova kutoka moyoni na pia nyinyi nyote kwa ajili ya makala hayo.

Y. S., Japani

Makala kama hizo hutusaidia kukabiliana kihisia na pia hutuimarisha kiakili, ili tuweze kufanya vyema zaidi. Tafadhali endeleeni kuandika makala kama hizo tunazohitaji ili tujielewe vizuri zaidi.

C. L., Marekani

Nilipimwa na kupatikana na mfadhaiko wa tukio lenye kutisha, lakini jambo nililofahamu tu kuhusiana na tatizo hilo ni kwamba mtu hukumbuka kwa ghafula tukio hilo lenye kutisha. Makala zenu zilieleza mambo yote kuhusu dalili zake. Nilifikiri huenda hali yangu ya kiroho ilikuwa imeshuka sana. Hata hivyo nilisaidiwa sana na lile wazo lililosema kwamba jambo la maana, si vile tunavyojiona, bali ni vile Yehova anavyotuona.

J. S., Japani

Sikuweza kuona habari hiyo kwa urahisi kwa sababu machozi yalinitoka nilipokuwa nikisoma. Kwa miaka miwili sasa nimekuwa nikiota ndoto mbaya kuhusu mambo yaliyotukia babu yangu alipokufa akiwa mikononi mwangu, alipougua mshtuko wa moyo. Nililia sana nilipokuwa katika mikutano ya Kikristo. Habari hiyo ilinisaidia kuelewa kwa nini ninaumia vibaya. Sasa ninajua mahali ambapo ninaweza kupata msaada—kwa Baba yangu wa kimbingu mwenye upendo anayejali sana na kupitia tengenezo lake.

P. T., Australia

Miaka mitano iliyopita mume wangu alikufa katika aksidenti ya gari, na mwaka mmoja baadaye nilianza kupata dalili zisizo za kawaida. Wakati nilipopokea makala hiyo nilihisi kabisa kuwa wale wanaoelewa hali yangu vizuri zaidi ni Yehova na tengenezo lake. Kuwa na maoni hayo kulinipa nguvu mpya za kuendelea. Ninashukuru kutoka moyoni kwa ajili ya kazi yote mnayofanya!

A. K., Japani

Usomaji wa Biblia Ninashukuru sana kutoka moyoni kwa ajili ya makala “Vijana Huuliza . . . Ninaweza Kufanyaje Usomaji wa Biblia Ufurahishe Zaidi?” (Agosti 22, 2001) Nina umri wa miaka 17. Nimeshindwa kusoma Biblia yote. Wakati fulani niliacha kuisoma kwa sababu tu nilikuwa na shughuli nyingi, na wakati mwingine kwa sababu nilifikiri kwamba lile nililokuwa nikisoma halingenifaidi kwa vyovyote. Hata hivyo vijana waliotajwa katika makala hiyo wanafurahia sana usomaji wao wa Biblia na kunufaika kutokana nao. Hata mimi nilitiwa moyo kuisoma na sasa ninajitahidi kuendelea bila kuacha.

Y. T., Japani