Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jitihada Yake Ilileta Thawabu

Jitihada Yake Ilileta Thawabu

Jitihada Yake Ilileta Thawabu

VIJANA WENGI MASHAHIDI WA YEHOVA HUWEKA mfano mzuri kwa kuzungumza kuhusu imani yao kwa ujasiri. Msichana mmoja aitwaye Stella kutoka Salonika, nchini Ugiriki anasema hivi: “Njia za kutumia video zetu ili kusaidia wengine kumjua Yehova zilizungumziwa kwenye mkutano wetu mmoja wa Kikristo. Nilifikiria jinsi ambavyo ningetumia video Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name. Siku iliyofuata nilizungumza na mwalimu mkuu, na kumwomba aonyeshe video hiyo shuleni. Alikubali kufanya hivyo maadamu tu walimu wangekubali.

“Baadaye siku hiyo, mwalimu mkuu aliniambia kuwa video hiyo ingeonyeshwa juma ambalo lingefuata baada ya shule. Nilivunjika moyo kwa sababu nilifikiri kwamba wanafunzi wenzangu hawangekubali kutumia wakati wao baada ya shule kutazama video hiyo. Hata hivyo, nilialika kila mmoja wao siku iliyofuata. Walikubali na hata wakawaalika wanafunzi kutoka madarasa mengine. Walimu sita—akiwemo mwanatheolojia—walikuja kutazama video hiyo pia.

“Wote waliitazama kwa makini. Baadaye, mwalimu mkuu akaniomba niongoze kipindi cha maswali kwa majibu. Wanafunzi wengi walivutiwa na kazi ya kujitolea inayofanywa katika makao makuu ya Mashahidi wa Yehova, ambayo ilionyeshwa katika video hiyo. Mwanafunzi mmoja alisema hivi: ‘Ingawa hawalipwi mshahara, wao hufanya kazi yao kwa shangwe!’

“Niliwaeleza wote waliohudhuria kuhusu vitabu vyetu vinavyotegemea Biblia. Pia, niligawanya trakti Habari za Ufalme Na. 36, yenye kichwa ‘Milenia Mpya—Unaweza Kutarajia Nini Wakati Ujao?’ Mwalimu mkuu aliomba nakala zaidi ili awape walimu ambao hawakuwepo.

“Baadaye, wanafunzi wengi waliwaeleza marafiki wao kuhusu video hiyo. Nilifurahi kwamba nilitumia nafasi hiyo kutoa ushahidi. Wanafunzi wenzangu sasa wananiheshimu zaidi, lakini jambo la maana hata zaidi ni kwamba wanamheshimu Mungu ninayemwabudu!”