Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Wasiwasi Ningependa kutoa shukrani zangu kwa ajili ya makala “Vijana Huuliza . . . Ninawezaje Kuacha Kuwa na Wasiwasi Mwingi Mno?” (Septemba 22, 2001) Nina umri wa miaka 17, na kila siku mimi huwazia jinsi maisha yangu yatakavyokuwa nitakapomaliza shule ya sekondari. Mimi huepuka kumweleza yeyote mahangaiko yangu kwa sababu sitaki kuwasumbua watu wengine, hivyo mimi huumia peke yangu. Makala hiyo ilinisaidia kuona umuhimu wa kuzungumza na mamangu na pia watu wengine wakomavu kutanikoni.

L. R., Marekani

Nina umri wa miaka 17. Mara nyingi mimi huwa na wasiwasi kuhusu afya ya mamangu, kazi yangu ya shule, na kazi za nyumbani. Siku zote mamangu hunigusa wakati shauri kuhusu wasiwasi linapotolewa katika mikutano ya Kikristo. Kwa hiyo nilithamini madokezo katika makala hiyo yaliyonisaidia kuona umuhimu wa kupangia wakati wangu na kufanya kazi ambazo hazinifurahishi badala ya kuziahirisha. Asanteni kwa makala hiyo.

H. H., Marekani

Nikiwa baba na mzee Mkristo, nimeona kwamba vijana wetu wanahangaikia wakati ujao. Shauri lenu la kuzungumzia mambo pamoja na wazazi na kushughulikia matatizo bila kukawia ni zuri. Asanteni kwa kuendelea kupendezwa na vijana wetu.

R. H., Kanada

Matineja Walioshuka Moyo Nilipewa mgawo shuleni wa kuandika insha kuhusu tatizo lolote la kijamii linalokabili vijana waliobalehe. Nilitumia kichwa cha ule mfululizo wa makala “Msaada kwa Matineja Walioshuka Moyo” katika toleo la Septemba 8, 2001. Kuna vijana wengi walioshuka moyo katika eneo ninaloishi. Nimewahi kutumia Amkeni! katika kazi nyingine za shule na nikapata maksi nyingi!

S. H., Australia

Mvulana wetu tineja aliugua moyo na ubongo. Ingawa ugonjwa ulitibiwa, hatari kubwa zaidi—kushuka moyo—haikutambuliwa. Mwana wetu alijiua. Ijapokuwa sasa hatuwezi kumsaidia, makala hiyo imetusaidia sana kuelewa tatizo lake. Tulishukuru sana kwa sababu tatizo hilo lilizungumziwa na kwamba mnawajali vijana wetu sana.

G. & G. R., Ujerumani

Wakati fulani mimi hushuka moyo sana na kuanza kuhisi sifai kitu. Niliona haya kuzungumza kuhusu hisia zangu pamoja na wazazi wangu Wakristo au hata wazee katika kutaniko. Hata hivyo, niliposoma sentensi iliyosema, “Si wewe uliyejiletea hali hiyo,” nilipata utulivu mwingi sana! Nilitambua kwamba si mimi peke yangu ninayekabili hali hiyo.

H. T., Japani

Kuutazama Ulimwengu Ninaandika ili kuwapongeza kwa ajili ya michoro yenye kuchekesha mnayoweka katika makala “Kuutazama Ulimwengu.” Michoro hiyo hunisaidia kukumbuka habari zinazoelezwa na, la maana zaidi, hunichekesha. Endeleeni kufanya kazi hiyo nzuri sana!

A.I.P.B., Hispania

Kalenda ya Wamaya Ninaamini niliona kosa katika makala “Wamaya—Walivyokuwa na Walivyo Leo.” (Septemba 8, 2001) Picha iliyo kwenye sanduku “Kalenda ya Wamaya” ni kalenda ya jua ya Waazteki. Kwa usahihi zaidi, ni sehemu ya kati ya kalenda hiyo inayoonyesha mungu wa jua wa Azteki.

R. S., Marekani

“Amkeni!” linajibu: Msomaji wetu anasema kweli. Inaonekana yule aliyetuuzia picha hiyo aliweka kibandiko kisichofaa. Kwa kusikitisha, kosa hilo halikutambuliwa kabla gazeti halijapelekwa kuchapishwa. Tunasikitika kwa kosa hilo.