Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Mandhari ya Ulimwengu Huu Inabadilika”

“Mandhari ya Ulimwengu Huu Inabadilika”

Njoo, Usikilize Hotuba ya Watu Wote

“Mandhari ya Ulimwengu Huu Inabadilika”

SIKU HIZI NI ZENYE MSUKOSUKO. Tukio moja la kushtua baada ya jingine hutokea haraka sana. Je, umewahi kuhisi kwamba umelemewa na kuvurugwa akili kwa sababu ya hayo yote—kwamba hali inabadilika haraka mno?

Biblia inasema jambo hili la kweli kuhusu shughuli za wanadamu: “Mandhari ya ulimwengu huu inabadilika.” (1 Wakorintho 7:31) Mtume Paulo, aliyeandika maneno hayo, alilinganisha matukio ya ulimwengu na jinsi mandhari za mchezo wa kuigiza jukwaani hubadilika. Tangu zamani za kale, viongozi wa ulimwengu na vilevile watu wanaoanzisha mitindo mipya wametokea na kutoweka. Mambo mapya huja na ya kale hupotea, tena na tena. Lakini katika wakati wetu, hasa tangu mwaka muhimu wa 1914, yaelekea mambo yanabadilika haraka zaidi.

Hata hivyo, je, unajua kwamba matatizo hayo ya ulimwengu, hata yale ya hivi majuzi, ni habari njema pia kwa wanadamu? Ndiyo, matukio hayo yanamaanisha kwamba hivi karibuni mandhari ya ulimwengu itabadilika kuwa nzuri. Zamani za kale Biblia ilitabiri kwamba wakati wetu ungekuwa wenye taabu nyingi. Biblia inaeleza pia kwamba misukosuko hiyo ingetangulia badiliko kuu kushinda mabadiliko yote yaliyowahi kutukia ulimwenguni. Ijapokuwa linaonekana kuwa lenye kutisha, badiliko hilo litakalokuja ni habari njema kwa watu wote wanyofu kotekote. Mandhari ya ulimwengu huu itabadilika na wanadamu wote wataishi kwa amani na furaha.

Je, ungependa kujua mengi zaidi juu ya mabadiliko hayo na kile ambacho Biblia inasema juu yake? Umekaribishwa kwa uchangamfu kuhudhuria hotuba ya watu wote yenye kichwa “Mandhari ya Ulimwengu Huu Inabadilika,” kwenye mojawapo ya makusanyiko ya wilaya ya Mashahidi wa Yehova yatakayoanza mwezi wa Agosti. Makusanyiko hayo yatafanywa katika sehemu nyingi ulimwenguni pote. Ili ujue kusanyiko litakalofanywa karibu na mahali unapoishi, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au ona toleo la Februari 15, 2002 la gazeti letu la Mnara wa Mlinzi.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Bomu la nyuklia linaharibu kabisa Hiroshima mwaka wa 1945

[Hisani]

USAF photo

[Picha katika ukurasa wa 32]

Ukuta wa Berlin unabomolewa mwaka wa 1989

[Hisani]

AP Photo/Lionel Cironneau

[Picha katika ukurasa wa 32]

Magaidi washambulia World Trade Center huko New York mwaka wa 2001