Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Viumbe Nina umri wa miaka 11, na ninawapenda sana wanyama. Nilipopokea mfululizo wa makala “Ni Nani Atakayelinda Viumbe?” (Novemba 22, 2001), nilikuwa na hamu sana ya kuisoma. Ninamsikitikia ndege aina ya wandering albatross, anayeonyeshwa katika ukurasa wa 7. Inahuzunisha kwamba ndege hao wanakufa maji kwa sababu ya kushikwa kimakosa na wavuvi. Pia nilipendezwa na picha ya mwisho katika ukurasa huo, ile ya taa wa maji safi. Tafadhali endeleeni kuandika makala kama hizo!

S. V., Marekani

Magereza Sijui namna ya kueleza nilivyohisi niliposoma makala “Masimulizi ya Imani Kutoka Gereza Maarufu.” (Novemba 22, 2001) Mwanangu yumo gerezani kwa sababu ya kuiba katika benki. Hii ni mara yake ya pili kufungwa gerezani. Nitamtumia makala hiyo. Ninasali kwamba itagusa moyo wake na kumtia moyo kuitikia upendo ambao Yehova anatuonyesha sote. Asanteni kwa faraja mnayotutolea.

C. M., Marekani

Kujiua Asanteni kwa mfululizo wa makala “Uhai Una Thamani.” (Oktoba 22, 2001) Wakati nilipokuwa katika shule ya msingi, nilipatwa na mfadhaiko mwingi sana. Yehova alinitegemeza sana kupitia Biblia na ushirika wa Kikristo. Lakini bado nilihisi kwamba sifai. Wakati niliposoma sanduku lenye kichwa “‘Je, Mungu Atanisamehe kwa Kuhisi Hivi?’” niliona ni kama Yehova mwenyewe alikuwa akiongea nami. Ni shangwe kujua kwamba Yehova hawezi kusahau watu kama mimi!

S. H., Japani

Ningependa kuwajulisha kwamba nilifurahi sana niliposoma mfululizo huo wa makala. Nilifurahi kwamba makala hizo hazikuwa na mashauri makali kwani niliposoma kichwa kwenye jalada nilifikiri kwamba ningeshauriwa vikali. Sanduku lenye kichwa “‘Je Mungu Atanisamehe kwa Kuhisi Hivi?’” lilinifanya karibu kulia. Kwa msaada wa makala hayo, niliweza kuzungumza na dada Mkristo kuhusu matatizo yangu. Asanteni kwa kushughulikia habari hiyo vyema.

A. F., Ufaransa

Nimesoma mfululizo huo wa makala mara nane. Nilipokuwa katika shule ya msingi, nilitaka kujiua. Nilitamani kufa. Makala hizo zilinisaidia kutambua kwamba ingawa kila siku sina furaha maishani, bado uhai una thamani. Mimi si mmoja wa Mashahidi wa Yehova, lakini kwa muda fulani nimekuwa nikisoma magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Nyinyi ni watu wa pekee sana!

S. M., Japani

Wanawake Wanaopigwa Asanteni kwa makala “Msaada kwa Wanawake Wanaopigwa.” (Novemba 8, 2001) Kichwa kwenye ukurasa wa 3—“Huenda Akabadilika Wakati Huu”—kinaonyesha tazamio ambalo nimekuwa nalo kwa miaka mingi. Ninaweza kuthibitisha uhakika wa yale mliyosema katika ukurasa wa 4, kwamba mara nyingi mkosaji huhurumiwa badala ya aliyekosewa.

S. M., Ujerumani

Mfululizo huo wa makala ulinichangamsha sana. Kama wengine walivyofanya bila shaka, nililia sana kuanzia niliposoma ukurasa wa kwanza kwa sababu nilikumbuka matatizo na uchungu niliovumilia wakati mmoja. Ninathamini wazo la kuwa Yehova anaona kila mmoja wetu kuwa wa maana. Nikiwa mhubiri wa wakati wote, nimetambua kuwa mahali ninapohubiri watu wengi wanapenda kusoma makala hizo, hivyo ilinibidi kuagiza magazeti zaidi. Asanteni sana kwa kuchapisha habari kama hiyo yenye thamani.

K. J., Australia

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 30]

Kipepeo: Butterfly House, Mittagong, Australia