Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Yabisi-Kavu Nilitiwa moyo sana niliposoma mfululizo wa makala wenye kichwa “Tumaini kwa Wale Wanaougua Yabisi-Kavu.” (Desemba 8, 2001) Nina umri wa miaka 21, na kwa miaka 15 hivi nimeugua ugonjwa wa yabisi-kavu na kuteseka kutokana na athari zake. Makala hizo zilinitia moyo sana, na zilinipa nguvu ya kuendelea kuvumilia.

A. F., Ufaransa

Mimi ni mhubiri wa wakati wote, na ninafurahia pendeleo hilo ingawaje inazidi kuwa vigumu kutimiza pendeleo hilo siku baada ya siku. Nilipimwa na kupatikana na yabisi-kavu aina ya osteoarthritis. Kila siku mimi huhisi maumivu, na wakati mwingine, hali hiyo hunifanya nishuke moyo. Asanteni kwa makala hiyo iliyokuja kwa wakati unaofaa, na pia asanteni kwa kutukumbusha kwamba faraja ya kweli inatokana na ahadi ya Yehova ya ulimwengu mpya.

H.M.A., Marekani

Nina ugonjwa wa baridi-yabisi, na sasa ninapata nafuu baada ya kuugua vikali hivi majuzi. Makala hizo zilieleza vizuri maumivu ambayo mgonjwa anayeugua baridi-yabisi huhisi. Nilijifunza mengi zaidi kuhusu ugonjwa huo na ninalohitaji kufanya ili kupunguza athari zake.

G.F.F., Ureno

Nina umri wa miaka 21, na nilipimwa na kupatikana na ugonjwa wa baridi-yabisi wa watoto nilipokuwa na umri wa miaka 10 tu. Nimesoma masimulizi ya wale waliougua ugonjwa huo katika magazeti ya kitiba, lakini hakuna yoyote ya masimulizi hayo yanayoweza kulinganishwa na kusoma kuhusu ndugu na dada zangu wa kiroho wanaokabiliana na hali sawa na yangu. Kama Katia, aliyetajwa katika makala hizo, mimi sikuweza kuendelea kuwa mhubiri wa wakati wote. Nilipata faida nyingi kwa kusoma jinsi ambavyo wengine wamekabiliana na mfadhaiko na hisia ya hatia kwa sababu ya kushindwa kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Yehova.

H. M., Marekani

Nilipokuwa na umri wa miaka 24, nilipimwa na kupatikana na ugonjwa wa baridi-yabisi, na sasa mwaka mmoja umepita. Ilinibidi niache utumishi wangu wa wakati wote. Nilishuka moyo sana. Kwa sababu ya uchungu mwingi na uchovu, sasa ninaweza kufanya tu nusu ya yale niliyokuwa nikifanya. Nimefarijiwa na makala hiyo kwa sababu nimejua kwamba wengine wanapatwa na maumivu ya mwili na kihisia kama mimi. Pia nilipendezwa na ushauri uliotolewa kwamba nifanye tu yale ninayoweza kutimiza. Ninatazamia wakati ambapo “mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu.”—Isaya 35:6.

T. U., Japani

Mwaka mmoja uliopita nilianza kuhisi maumivu makali katika viungo vyangu. Kwa sababu nina umri wa makamo, sikufikiri ningekuwa na ugonjwa wa yabisi-kavu. Makala hiyo ilinisaidia kuona uhitaji wa kuwa na usawaziko na kuwa mwenye kiasi kuhusu mambo ninayotazamia kutimiza.

B. P., Marekani

Nina umri wa miaka 19, na viganja vyangu, viwiko vyangu vya miguu, na magoti yangu yameathiriwa na yabisi-kavu. Nilipendezwa hasa na kichwa kidogo kilichosema “Ishi kwa Kupatana na Hali Yako.” Nilihama Marekani na kuja Ekuado ili niwe mhubiri wa wakati wote huku. Lakini kwa sababu ya unyonge, uchovu, na uchungu, ninaweza kwenda kwenye utumishi kwa muda mfupi tu. Nimeamua kurudi nyumbani ili nipate matibabu na ninatumaini kurudi hapa Ekuado nitakapopata nafuu.

J. S., Ekuado

Fêng Shui Asanteni kwa makala “Je, Wakristo Wanapaswa Kushiriki Desturi ya Fêng Shui?” (Desemba 8, 2001) Mimi ni msanii wa mapambo ya nyumba, na hivi majuzi mteja mmoja alitaka nitumie desturi ya fêng shui katika kazi hiyo. Nilisita kufanya hivyo, kwa kuwa sikufahamu mengi kuhusu desturi hiyo. Makala hiyo ilikuja kwa wakati unaofaa! Sasa nimeamua kwamba sitatumia desturi hiyo katika kazi ya kuunda mapambo.

C. V., Marekani