Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mwongozo Unaotegemeka kwa Ajili ya Wakati Ujao

Mwongozo Unaotegemeka kwa Ajili ya Wakati Ujao

Mwongozo Unaotegemeka kwa Ajili ya Wakati Ujao

JE, KUTOTEGEMEKA kwa ubashiri wa kutumia namba na aina nyinginezo za uaguzi kunamaanisha kwamba hatuwezi kamwe kujua mambo ya wakati ujao? La hasha!

Wanadamu hawawezi kujua mambo ya wakati ujao kupitia namba. Lakini “Mungu aliye hai,” ambaye anatangaza “mwisho tangu mwanzo” amewajulisha mambo ya wakati ujao. Naye huwajulisha kupitia Neno lake, Biblia. (1 Timotheo 4:10; Isaya 46:10) Isitoshe, neno la Mungu aliye hai ‘linaweza kufahamu fikira na makusudio ya moyo’ na hivyo kukusaidia kujua nia yako na mambo yanayoweza kukufanya ufanikiwe, lakini neno la wabashiri wanaotumia namba haliwezi kufanya hivyo.—Waebrania 4:12.

Muumba wetu, ambaye ni Mtungaji wa Biblia, ndiye tu anayeweza kutabiri kwa usahihi mambo ya wakati ujao. Mungu ana nguvu zisizo na kifani, naye hutumainika sikuzote. Yehova Mungu alisema hivi: “Nimenena, nami nitafanya.” (Isaya 46:11) Baada ya kuwaongoza Waisraeli kuingia Nchi ya Ahadi, Yoshua alisema hivi kwa uhakika: “Halikuanguka neno lo lote katika jambo lo lote lililokuwa ni jema ambalo BWANA alikuwa amelinena katika habari ya nyumba ya Israeli; yalitimia mambo yote.”—Yoshua 21:45; 23:14.

Biblia ina unabii mwingi ambao haujatimizwa. Baadhi ya unabii huo unatabiri kwamba uovu utaondolewa kabisa ili dunia iwe paradiso. (Zaburi 37:10, 11; Mithali 2:21, 22) Je, unavutiwa na wakati ujao wa aina hiyo? Je, unaamini kwamba Muumba wetu ana hekima na nguvu za kuboresha hali duniani? Ikiwa ndivyo, utafurahia kujua yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali ya wakati ujao ya dunia. *

Kwa hiyo, badala ya kutafuta habari zako za wakati ujao katika namba, tumia wakati wako kwa hekima sasa kwa kujitahidi kupata ujuzi sahihi wa Biblia na unabii uliomo. Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia kupata ujuzi zaidi kuhusu wakati ujao unaotajwa na Neno la Mungu, Biblia.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 5 Ona sura ya 1, 10, na 19 ya kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.