Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Usalama Kazini Asanteni sana kwa mfululizo wa makala “Je, Uko Salama Kazini?” (Februari 22, 2002) Siku moja tu kabla ya kusoma makala hizo, kulikuwa na hali ya kutoelewana mahali ninapofanya kazi. Ushauri wenu wa kuitikia kwa upole, unaopendekezwa katika gazeti lenu, ni mzuri sana. Habari iliyoonyesha hatari za kufanya kazi kuanzia asubuhi na mapema hadi usiku sana, ilifaa pia. Hivi majuzi nilishurutishwa kukubali kazi ya aina hiyo, lakini niliikataa. Niliposoma gazeti hilo, nilifurahi sana kwa sababu nilikuwa nimefanya uamuzi mzuri!

M. H., Japan

Vijana Huuliza Nimemaliza tu kusoma makala “Vijana Huuliza . . . Nifanye Nini Nikikutana na Mwanafunzi Mwenzangu?” (Februari 22, 2002) Nikiwa mhubiri wa wakati wote na mwanafunzi katika shule ya upili, mimi huhisi kama Simon aliyetajwa katika makala hiyo. Nimehofia kukutana na wanafunzi wenzangu ninapokuwa kwenye utumishi. Kikumbusha hicho kizuri sana kilitoka kwa Yehova na ninamshukuru.

S. S., Marekani

Nina umri wa miaka 14, na nilihofu kukutana na wanafunzi wenzangu katika eneo nililohubiri. Nilifarijika kujua kwamba Yehova hunisaidia ninapobisha milango. Makala hiyo ilinitia nguvu.

M. L., Italia

Chingamu Asanteni sana kwa makala “Kutafuna Chingamu Ni Zoea la Kisasa na la Kale.” (Februari 22, 2002) Ninapenda kutafuna chingamu, lakini kila mara huimeza bila kukusudia. Makala hiyo ilinionya nisimeze chingamu. Nitafuata ushauri wenu!

K. B., Thailand

Wamasai Asanteni sana kwa makala “Wamasai Ni Watu wa Pekee Wanaovutia.” (Februari 22, 2002) Nimetamani kutembelea Kenya tangu nilipokuwa mdogo, na bado nina tamaa hiyo. Ingawa nimefanya utafiti mwingi kuhusu desturi na mapokeo ya Wamasai, sikufikiri wengine ni Mashahidi wa Yehova. Sasa mimi ni mhubiri wa wakati wote, na ninatamani kuhudhuria kusanyiko nchini Kenya. Tafadhali endeleeni kuchapisha habari kuhusu Afrika.

Y. H., Japan

Pomboo Nina umri wa miaka 14, na ninawashukuru sana kwa makala “Kutafuta Pomboo Huko New Zealand.” (Januari 8, 2002) Makala hiyo ilinisisimua sana. Habari hiyo ni nzuri sana na inaonyesha jinsi Yehova alivyo na nguvu nyingi kwa kuwa aliwaumba viumbe hao wa ajabu wenye akili. Ninapendezwa sana na pomboo, na ninatazamia wakati ambapo nitaweza kuwajua vizuri zaidi katika ulimwengu mpya wa Mungu.

A. C., Australia

Nina umri wa miaka 15, na ninawapenda sana wanyama. Ninapendezwa hasa na pomboo, ambao huogelea kwa fahari sana. Niliposoma makala hiyo, nilimshukuru Yehova Mungu. Nitalinda mazingira na wanyama ambao ameumba.

A. N., Japan

Majibu ya Wahariri wa Amkeni! Ninawapongeza kwa majibu yenu yanayotokea mara kwa mara katika makala ya “Kutoka kwa Wasomaji Wetu.” Mhariri wa gazeti la kwetu hutoa majibu makali, yenye matusi na ya kukejeli, hata gazeti lake linapokosea. Ninapendezwa na majibu ya Amkeni! ambayo, ingawa yanaonyesha kwamba wahariri hujivunia gazeti lao, majibu yao huonyesha wanawajali wasomaji.

K. W., Marekani