Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Ibada Kabla ya kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, sikuweza kamwe kueleza jinsi nilivyohisi kumhusu Mungu. Mfululizo wa makala “Je, Nimwabudu Mungu Jinsi Nipendavyo?” (Aprili 22, 2002) waeleza vizuri sababu zilizonichochea kujifunza Biblia. Nimepanga kumtumia kila mmoja katika familia yetu nakala moja.

B. R., Marekani

Simulizi la Maisha Nililia machozi ya shangwe na huzuni vilevile niliposoma simulizi la “Licha ya Majaribu, Tumaini Langu Halijafifia.” (Aprili 22, 2002) Ujasiri wa Ndugu Hanák akiwa na umri wa miaka 20 ulinikumbusha kwamba twaweza kumtegemea Yehova awape hata vijana azimio la kushikilia viwango vya uadilifu vya Yehova. Asanteni kwa kuendelea kuchapisha makala nzuri kama hizo zinazotupa sisi kichocheo tunachohitaji katika nyakati hizi za hatari tunamoishi.

K. G., Marekani

Vijana Huuliza Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 11, na nataka kuwashukuru kwa makala “Vijana Huuliza . . . Nifanye Nini Nikikutana na Mwanafunzi Mwenzangu?” (Februari 22, 2002) Nilijipata katika hali kama ya vijana wanaoelezwa katika makala hiyo. Baada ya kuisoma, nilielewa kwamba sipaswi kuaibikia ujumbe wa haraka na wenye thamani tunaopelekea watu. Asanteni sana kwa habari hiyo.

D.D.S., Italia

Nina umri wa miaka 10. Asanteni kwa makala hiyo. Baada ya kuisoma, nilikwenda katika huduma ya shambani siku iliyofuata na sikuwa na wasiwasi kwa sababu ya kutumia ushauri uliokuwa katika gazeti hilo.

D.D.C., Italia

Ni kana kwamba makala “Vijana Huuliza . . . Mbona Yule Ninayeishi Naye Ni Mgumu Sana?” (Aprili 22, 2002) iliandikwa kwa ajili yangu! Mimi ni mtumishi wa wakati wote, na nimeishi na mwenzangu kwa miezi sita. Kama makala hiyo inavyoonyesha, kuishi na mtu wa malezi tofauti kwaweza kuwa jambo lenye kupendeza na pia kwaweza kusababisha mfadhaiko. Kwa msaada wa wazazi wangu, wazee, na Yehova, nimebadili mtazamo wangu polepole. Sasa tunatamani kuhamia kutaniko lenye uhitaji mkubwa zaidi nikiwa na mwenzangu. Nafikiri Yehova alitoa makala hii kama zawadi kwangu!

I. S., Japan

Makala “Vijana Huuliza . . . Naweza Kuwahubiria Wanashule Wenzangu Vipi?” (Machi 22, 2002) ilikuwa ya pekee kwangu. Nakumbuka nikisitasita kuhubiria wanafunzi wenzangu hasa rafiki mmoja ambaye alistahi imani yangu. Hatukuonana kwa muda mrefu hadi miaka kadhaa baadaye nilipogundua kwamba alikuwa akijifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Leo sisi sote ni wazee wa makutaniko na marafiki wakubwa. Kama vile makala hiyo ilivyoonyesha, kuongea na wengine juu ya Yehova huleta matokeo mazuri.

J.R.M., Brazili

Yanaelimisha Watu wa Kila Umri Mimi hufurahia magazeti yenu kwelikweli kwa sababu yananipendeza sana na pia yanapendeza watoto wangu. Magazeti mengi yanaharibu vijana wetu. Lakini nyinyi hufanya vijana wetu wawe watu wema. Asanteni kwa elimu mnayotupatia.

G. M., Urusi