Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia—Neno la Mungu Au la Binadamu?

Biblia—Neno la Mungu Au la Binadamu?

Biblia​Neno la Mungu Au la Binadamu?

ULIMWENGU WA LEO una matatizo mengi sana. Ndoa zinavunjika. Ujeuri katika familia umeenea. Mamia ya mamilioni ya watu hawana chakula cha kutosha. Uhalifu unaongezeka hata usiweze kudhibitiwa. Ni vigumu kupata amani na usalama. Kwa nini ulimwengu uko hivi? Je, kuna utatuzi wowote?

Biblia inaandaa majibu ya maswali hayo na vilevile inaandaa mwongozo katika maisha ya kila siku. Basi, je, hatupaswi kupendezwa na yale ambayo Biblia inasema?

Watu wengine hufikiria kwamba Biblia ni kitabu tu cha mkusanyo wa ngano, hekaya, na hekima ya watu. Hata hivyo, wengine huiona Biblia kuwa Neno la Mungu lililopuliziwa. Ni maoni gani yaliyo sahihi? Kitabu hiki Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? kitakusaidia kulijibu swali hilo. Tunakuomba uyafikirie mwenyewe mambo haya ya hakika. Huenda kufanya hivyo kukabadili maisha yako milele.

Unaweza kujaza kuponi iliyo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Onyesha lugha unayotaka.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Alexander the Great: Roma, Musei Capitolini