Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ilipeperushwa na Upepo

Ilipeperushwa na Upepo

Ilipeperushwa na Upepo

Mwanamume mmoja alikuwa akitembea katika barabara ya Mumbai, India, alipoona karatasi yenye maandishi iliyopeperushwa na upepo miguuni mwake. Ilikuwa trakti Habari za Ufalme Na. 36, yenye kichwa “Milenia Mpya—Unaweza Kutarajia Nini Wakati Ujao?” Kichwa hicho kilimvutia. Mara moja aliiokota na kuisoma yote. Alipendezwa na akaomba Biblia na vichapo vingine kwa kuwa alitaka kupata habari zaidi.

Karatasi hiyo, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova, ina mambo yenye kuimarisha imani. Inaeleza kwamba matatizo tunayokabili, kutia ndani magonjwa, umaskini, na vita yanasababishwa na “pupa, kutoaminiana, na ubinafsi—tabia ambazo utafiti wa kisayansi, tekinolojia, au siasa peke yake haziwezi kuondoa.” Trakti hiyo inaonyesha pia kwamba hivi karibuni, Mungu ataondoa uovu wote duniani.

Je, ungependa kujifunza yale ambayo Biblia inaahidi kuhusu wakati ujao? Mashahidi wa Yehova hufundisha mamilioni ya watu Biblia nyumbani mwao, wakitumia vichapo vya Biblia, kama kichapo Mungu Anataka Tufanye Nini? Kichapo hicho hujibu maswali kama: Mungu ni Nani? Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Dunia? Ufalme wa Mungu ni Nini? Biblia inawezaje kuboresha maisha yako ya familia?

Ukipenda, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukutembelea nyumbani mwako ili wakusaidie kuelewa yale ambayo Mungu atafanya hivi karibuni na watakueleza mengi kuhusu Ufalme wa Mungu. Tafadhali jaza kuponi iliyo hapa ili waweze kukusaidia.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.