Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kushuka Moyo Baada ya Kujifungua Ninawa shukuru sana kwa makala yenye kichwa “Nilipambana na Ugonjwa wa Kushuka Moyo Baada ya Kujifungua.” (Julai 22, 2002) Nilipata mtoto mwaka mmoja na miezi mitatu iliyopita. Utu wangu ulibadilika ghafula. Nyakati nyingine niliwaudhi wapendwa wangu kwa kuwa sikuelewa tatizo langu. Sasa nimeanza kupata nafuu. Makala hiyo ilinisaidia.

A. P., Rumania

Baada ya kusoma makala hiyo, mwanafunzi wangu wa Biblia alinidokezea kwamba ana ugonjwa huo. Sasa, yeye huenda hospitalini kila juma, na dawa anazopewa humsaidia kuendelea na shughuli zake za kawaida kwa furaha.

A. M., Japan

Yehova alijibu sala zangu kwa kuandaa makala hii. Ndugu wapendwa, kweli mwajua mahitaji ya dada zenu. Nilipopokea makala hiyo, nilihisi ni kana kwamba nimekumbatiwa kwa upendo na Yehova na tengenezo lake.

C. W., Marekani

Ninaendelea kupata nafuu kutokana na ugonjwa wa kushuka moyo baada ya kujifungua, na makala hiyo ilinitia moyo na kunipa nguvu. Mlieleza wazi kabisa jinsi ambavyo wale wanaougua ugonjwa huo huhisi. Nitaliweka gazeti hilo la Amkeni! mahali salama ili nisome madokezo yake mazuri ninapohitaji kitia-moyo.

E.V.F., Brazili

Hakuna makala nyingine ambayo imewahi kunigusa moyo kama makala hiyo. Ndoa yangu ilivunjika kwa sababu ya ugonjwa huo. Sasa binti yangu ana miaka mitano na ninampenda sana. Ilinichukua muda wa miaka mitatu hivi kushinda tatizo hilo.

A. O., Puerto Riko

Nilikuwa nikipambana na ugonjwa huo wa kushuka moyo kwa miezi mitatu. Nilipoambiwa kwamba gazeti la karibuni la Amkeni! lilizungumzia ugonjwa huo, nililia sana hata singeweza kuongea. Hakuna makala nyingine ambayo nimewahi kusoma inayozungumzia ugonjwa huo vizuri zaidi kama makala hiyo. Ninamshukuru Yehova na tengenezo lake kwa kututunza vizuri sana!

A. L., Kanada

Vijana Huuliza Ninawashukuru kwa moyo wangu wote kwa makala yenye kichwa “Vijana Huuliza . . . Ninaweza Kufanya Nini ili Niwe Mwenye Kuvutia Zaidi?” (Julai 22, 2002) Nina umri wa miaka 22, na makala hiyo ilinisaidia kuboresha utu wangu. Mradi wangu wa kwanza ni kujifunza kuwa mpole. Jambo muhimu hata zaidi ni kwamba ninataka nivutie machoni pa Yehova. Tafadhali endeleeni kuandika makala nzuri kama hizo.

A. H., Japan

Makala hiyo ilinigusa moyo. Nina umri wa miaka 18, na nyakati nyingine mimi husahau umuhimu wa kukuza sifa za kiroho. Kuanzia sasa na kuendelea, nimeazimia kukuza matunda ya roho kwa msaada wa Yehova.—Wagalatia 5:22, 23.

M.R.A., Brazili

Kwa muda wa miaka miwili, nimekuwa nikijiuliza kama watu wananiona kuwa mrembo. Nyakati nyingine nilihisi kuwa mimi si mrembo. Baada ya kusoma makala hiyo, nilifurahi sana kujua kwamba ninaweza kuvutia machoni pa Mungu mradi niwe mtumishi wake, na hilo ndilo jambo muhimu zaidi.

I. P., Marekani