Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Takataka Asanteni sana kwa makala zenye kichwa “Je, Tutazama Katika Takataka?” (Agosti 22, 2002) Mtu akiishi katika nchi yenye viwanda vingi, ni rahisi kuwa na “mazoea ya kutupatupa vitu.” Makala yenu ilinifanya nifikirie hatari za kufanya hivyo. Kuanzia sasa na kuendelea, nitafikiria kwa uzito kabla ya kutupa vitu!

J. B., Marekani

Nilifurahia sana makala zilizozungumzia tatizo la takataka. Kwa muda mrefu, niliishi katika ghorofa kubwa yenye mapipa kadhaa ya takataka. Siku moja nilipokuwa nikitembea nje niliona mashine mpya kabisa ya kutengenezea kahawa kwenye pipa lililojaa takataka. Hapo awali, vijana wawili waliniambia kwamba waliokota saa ya dhahabu mahali hapo. Nilishangaa kuona vitu vilivyotupwa humo. Sasa kuna kibao kinachosema, “Usichakure-chakure kwenye mapipa.”

B. Q., Marekani

Upasuaji wa Kubadili Sura Nawashukuru kwa moyo wangu wote kwa makala “Vijana Huuliza . . . Je, Nifanyiwe Upasuaji wa Kubadili Sura?” (Agosti 22, 2002) Nina umri wa miaka 14, na wanafunzi fulani shuleni hunifanyia mzaha kwa sababu ya sura yangu. Nilikuwa nimeazimia kuirekebisha. Makala hiyo ilinisaidia kuchunguza nia yangu na kuona jinsi nilivyokuwa nimekosea. Jambo la maana machoni pa Yehova ni utu wa ndani.

C. T., Ufaransa

Miezi kadhaa iliyopita, nilizungumza na mfanyakazi mwenzangu kuhusu upasuaji wa kubadili sura. Alihisi kwamba jambo hilo halikufaa kwa sababu ni kutomheshimu Muumba. Wakati huo, sikupata jambo lolote hususa katika vichapo vyetu kuhusu jambo hilo. Hata hivyo, nilimweleza kanuni za Biblia ambazo zingefaa nilizopata baadaye katika makala hiyo. Nilipomwonyesha makala hiyo, alifurahi sana.

M. R., Marekani

Rangi Ilikuwa rahisi kupaka nyumba yangu rangi baada ya kusoma makala “Kupaka Rangi Mpya.” (Agosti 22, 2002) Nawashukuru sana kwa makala hiyo iliyonisaidia kuokoa pesa zangu!

R. M., Marekani

Kuvutia Nina umri wa miaka 21 nami nahangaika sana kwa sababu najiona kuwa sivutii. Hisia zangu ni kama tu za Tyler kwenye makala “Vijana Huuliza . . . Ninaweza Kufanya Nini Ili Niwe Mwenye Kuvutia Zaidi?” (Julai 22, 2002) Nilihitaji hasa shauri la Biblia lenye kufaa katika makala hiyo. Asanteni kwa kichapo hiki na vinginevyo ambavyo huendelea kusaidia vijana ambao wanapatwa na matatizo mengi katika ulimwengu huu mwovu. Kilichobaki tu ni kutumia shauri hilo maishani mwangu.

P. L., Zambia

Sala Pokeeni shukrani zangu za kutoka moyoni kwa makala “Maoni ya Biblia: Sala Ambazo Mungu Husikia.” (Septemba 8, 2002) Siku nilipoisoma nilikuwa nimeshuka moyo sana. Ilinitia moyo sana kusoma maneno ya Isaya 41:10. Nafurahi sana kwamba Yehova huniimarisha mimi na pia wengine na kwamba yeye husikia sala zetu zote na hata mawazo yetu! Kwa miaka 20 nimekuwa nikiishi katika nyumba iliyogawanyika kidini. Maisha yangu yamekuwa magumu sana kwa sababu nimekuwa na ugonjwa wa kudumu kwa zaidi ya miaka 30. Asanteni sana kwa magazeti haya mazuri ajabu. Yanaendelea kuniimarisha kuvumilia.

D. G., Ujerumani