Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Ninataka Kujua Mengi Zaidi Kumhusu Yehova”

“Ninataka Kujua Mengi Zaidi Kumhusu Yehova”

“Ninataka Kujua Mengi Zaidi Kumhusu Yehova”

Ndivyo alivyoandika Miki mwenye umri wa miaka 12 kutoka Japani, ambaye alikuwa amemaliza tu kujifunza broshua Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha. Katika barua aliyowaandikia wachapishaji alisema, “nilipoona maneno ‘Maisha Yenye Kuridhisha,’ nilifikiri kwamba ilikuwa tu na ushauri wa jinsi ya kufanya maisha yawe yenye kuridhisha. Lakini nilipokuwa nikijifunza broshua hiyo nilitambua kwamba inatufundisha kuhusu nguvu na utukufu wa Mungu. Niliweza kuelewa kwa njia yenye kupendeza nguvu na utukufu wa Mungu na ninalopaswa kufanya ili niwe na maisha yenye kuridhisha. Kwa kuwa nimemaliza kujifunza broshua hiyo, ninatamani kujifunza mengi zaidi kumhusu Mungu na kupata maisha yenye kuridhisha. Tafadhali pokeeni shukrani zangu za kutoka moyoni kwa ajili ya kuchapisha broshua hii.”

Ikiwa ungependa kupokea nakala ya broshua Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, tafadhali jaza kuponi iliyo hapa chini na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya broshua Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.