Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mashauri Yanayofaa kwa Vijana

Mashauri Yanayofaa kwa Vijana

Mashauri Yanayofaa kwa Vijana

Bill, ambaye ni Shahidi wa Yehova, alikuwa akitoa magazeti karibu na mahakama moja huko California, Marekani, wakati alipokutana na mwanamume mmoja aliyetaka kuona magazeti yote ya Amkeni! ambayo alikuwa nayo. Bill anasema hivi: “Kwa kuwa wengine katika kutaniko walikuwa wamenipa magazeti ya zamani, nilimwonyesha mwanamume huyo magazeti mbalimbali.

“Mwanamume huyo alichagua magazeti mengi ambayo hakuwa amesoma na akayapanga pamoja. Alitaka kubaki na magazeti yote hayo. Alisema kwamba anafanya kazi katika mahakama ya wilaya na kwamba kazi yake ilikuwa kuwashauri vijana wenye matatizo. Alieleza kwamba yeye huchukua magazeti ya Amkeni! ili apige fotokopi makala za ‘Vijana Huuliza.’ Kisha yeye huzipanga katika faili kulingana na vichwa mbalimbali na kuwagawia vijana wanaokuja kushauriwa. Mwanamume huyo alisema: ‘Makala hizo huzungumzia matatizo yanayowapata vijana leo.’ Aliwapongeza Mashahidi wa Yehova kwa kuchapisha habari hizo nzuri za kuwasaidia vijana. Pia alisema kwamba atanitafuta baada ya majuma kadhaa ili apate magazeti mapya ya Amkeni!”

Habari nyingi zinazochapishwa katika makala za “Vijana Huuliza” zinapatikana katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Unaweza kuomba kitabu hicho chenye kurasa 320 kwa kujaza na kutuma kuponi iliyo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.