Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Njoo Usikilize Hotuba ya Watu Wote Yenye Kichwa “Ni Nani Wanaomtukuza Mungu Leo?”

Njoo Usikilize Hotuba ya Watu Wote Yenye Kichwa “Ni Nani Wanaomtukuza Mungu Leo?”

Njoo Usikilize Hotuba ya Watu Wote Yenye Kichwa “Ni Nani Wanaomtukuza Mungu Leo?”

Kumtukuza Mungu ni jambo linaloweza kuwashtua watu wa dini. Je, Mungu si Mwenye Enzi wa ulimwengu wote mzima? Basi, inawezekanaje mwanadamu wa hali ya chini amtukuze? Inawezekana, kwa sababu Biblia inatuhimiza ‘tumhofu Mungu na kumpa utukufu.’ (Ufunuo 14:7) Njia moja ambayo twaweza kufanya hivyo ni ‘kusikia neno la Mungu na kulishika.’ (Luka 11:28) Kwa kweli, tunapojifunza Biblia na kuishi kupatana na kanuni zake, tunamheshimu na kumtukuza Mtungaji wake, Yehova Mungu.

Lakini ni nani leo wanaomtukuza Mungu kwa njia hiyo? Mabilioni ya watu hudai kwamba wanafuata dini. Lakini je, kufuata dini tu ndiyo kumtukuza Mungu? Tunawezaje kuwa na hakika kwamba ibada yetu inampendeza Mungu na hivyo kumtukuza? Maswali hayo yatajibiwa katika hotuba ya kusisimua yenye kichwa “Ni Nani Wanaomtukuza Mungu Leo?” Hotuba hiyo ya watu wote itatolewa kwenye makusanyiko ya wilaya ya Mashahidi wa Yehova yanayoanza mwezi huu. Mamia ya makusanyiko hayo yatafanywa ulimwenguni pote. Ili ujue kusanyiko lililo karibu nawe, wasiliana na Mashahidi wa Yehova mahali unapoishi, au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili. Toleo la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 2003 lina orodha ya mahali pa makusanyiko katika nchi ya Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Tanzania, na Kongo (Kinshasa).