Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Ugaidi Nina umri wa miaka 15, na ninawashukuru kwa mfululizo wa makala wenye kichwa, “Je, Kuombea Amani Kwaweza Kumaliza Ugaidi?” katika toleo la Oktoba 22, 2002. Nimefadhaika sana tangu majengo ya World Trade Center yaliposhambuliwa mnamo Septemba 11, 2001. Kisa hicho hunihuzunisha sana. Ninatazamia siku ambayo Yesu, Mwana-Mfalme wa Amani, atatulinda sote. Tunaweza kufarijiwa sana na jambo hilo.

A. M., Marekani

Vyombo vya Zeppelin Makala yenye kichwa, “Vyombo vya Angani Vyenye Kusisimua,” katika toleo la Oktoba 22, 2002, ilinivutia sana kwani ilinikumbusha maisha yangu ya utotoni. Nilisomea katika pwani ya mashariki ya Uingereza. Siku moja nilipokuwa na umri wa miaka kumi, nilitazama chombo kimoja kama hicho kikipita polepole angani. Wanafunzi wote darasani walikimbia nje ili kuona chombo hicho chenye kustaajabisha. Sijasahau kamwe pindi hiyo, na makala yenu ilinikumbusha tukio hilo.

R. W., Uingereza

Baba yangu alikuwa rubani wa mojawapo ya vyombo vikubwa zaidi vya angani. Nimewahi kusafiri kwa chombo hicho mara mbili na ninapenda sana historia ya vyombo hivyo. Nilifurahi sana kwamba mlionyesha wazi tofauti iliyopo kati ya “chombo kisicho thabiti,” na “chombo cha zeppelin” kwa sababu watu wengi hawavitofautishi.

R. P., Marekani

Pengwini Mume wangu hakuwaruhusu wanangu kujifunza Biblia. Hivyo, wavulana hao hawapendi Biblia. Lakini makala zenu hunisaidia kuwafundisha mambo ya kiroho. Mimi huteua makala zinazoweza kuwapendeza ambazo hazizungumzii Biblia wala kumhusu Mungu. Kwa mfano, nilipiga fotokopi makala yenye kichwa “Tazama! Gwaride la Pengwini Wadogo” (Oktoba 22, 2002) na nikaiweka katika faili ndogo ambayo nimetengeneza inayoitwa Maajabu ya Uumbaji. Ninasali kwamba Yehova atabariki jitihada zangu za kuwasaidia wapendwa wangu wapate ukweli.

J. G., Ufaransa

Simu za Mkononi Makala ya “Vijana Huuliza . . . Je, Ninahitaji Simu ya Mkononi?” (Oktoba 22, 2002) ilinisaidia sana. Kabla sijasoma makala hiyo, singeweza kulala kabla ya kujibu ujumbe niliokuwa nimetumiwa. Lakini sasa mmenisaidia kuona faida na hasara za simu ya mkononi.

C. A., Ufilipino

Vijana wengi katika shule yetu wana simu za mkononi, kwa hiyo nilitaka pia kuinunua. Kwa kuwa nimesoma makala hiyo, nitafikiria sana faida za kuwa nayo na kuona ikiwa nitaitumia kwa busara. Ninahisi kwamba Yehova aliandaa makala hiyo kwa ajili yangu.

M. F., Japan

Nilikuwa nikitumia simu yangu kumtumia mvulana mmoja barua-pepe. Tulizungumzia matatizo yetu, na nilifurahi kwamba ningeweza kumweleza mambo yangu ya siri. Baada ya muda, aliacha kunitumia barua-pepe na nikakasirika. Lakini makala hiyo ilinionyesha kwamba kutuma barua-pepe ni namna ya kutafuta uchumba. Na ninaamini kwamba mvulana huyo alitambua jambo hilo pia. Sasa mimi hutoa anwani yangu ya barua-pepe kwa wale tu wanaoihitaji.

Y. M., Japan

Vijana Walioshuka Moyo Nina umri wa miaka 17 na ninapenda sana magazeti yenu. Wakati mmoja nilipokuwa hospitalini, niliona magazeti ya Amkeni! yakiwa yamewekwa kwenye rafu moja. Nilijifunza kwamba Mungu Mweza-Yote ana jina, anaitwa Yehova. Nilifurahia sana makala zenye kichwa “Msaada kwa Matineja Walioshuka Moyo.” (Septemba 8, 2001) Makala hizo zilinifaidi na kunisaidia kushughulikia matatizo yangu kwani wakati huo nilikuwa nimeshuka moyo. Asanteni kwa magazeti hayo mazuri na yenye kuelimisha. Ninawathamini sana.

G. Z., Urusi