Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoa Msaada Nawaandikia kuwajulisha kwamba nilithamini sana makala yenye kichwa “Upendo Waonyeshwa Kupitia Kazi Kubwa ya Kutoa Msaada.” (Novemba 22, 2002) Mafuriko yalipoanza huko Houston, Texas, katika Juni 2002, ndugu yangu alikuwa amelazwa hospitalini akiwa amepoteza fahamu kwa sababu ya kuugua maradhi ya moyo. Nyumba yake iliharibiwa vibaya na mafuriko hayo. Lakini ndugu zetu Wakristo walianza kurekebisha nyumba yake akiwa bado katika hali hiyo. Walitoa mazulia na kurekebisha kuta zilizoharibiwa na maji na kuitia nyumba yake dawa. Msaada wao uliniwezesha kumtembelea ndugu yangu hospitalini. Hatimaye alipata fahamu. Upendo na shukrani zangu zote kwa Yehova na tengenezo lake la ajabu haziwezi kuelezwa kupitia barua hii fupi.

P. H., Marekani

Nataka kuelezea uthamini wangu kwa kupata pendeleo la ajabu la kuwa miongoni mwa akina ndugu wenye upendo na wanaojali sana. Inasisimua kuona vile ndugu walivyotumia wakati na mali zao kuwasaidia wale walioathiriwa na mafuriko. Kwa kweli walionyesha upendo wa Kikristo.

A. M., New Zealand

Uhuru wa Kidini Mtu fulani alinipatia gazeti la Amkeni! la Juni 22, 2002, lenye makala yenye kichwa “Ufalme Uliotetea Uhuru wa Kidini Kujapokuwa Upinzani.” Kwa kuwa alijua ninaamini kwamba Mungu ni mmoja tu, alifikiri kwamba ningelipenda. Hakukosea. Nilisomea nchini Marekani na nikapata kumjua Dakt. Earl Morse Wilbur (aliyetajwa kwenye makala hiyo). Pia nimehudhuria mihadhara mingi kuhusu historia ya watu wanaoamini kwamba Mungu ni mmoja tu. Hata hivyo, singeweza kuandika makala inayoeleza jambo hilo vizuri kama ile yenu!

M. M., Jamhuri ya Cheki

Kusakamwa Koo Kwenye sehemu ya “Kutoka kwa Wasomaji Wetu” katika gazeti la Amkeni! la Novemba 22, 2002, nilishangazwa na majibu ambayo mlimpa msomaji aliyeandika kwamba soseji zinaweza kuwasakama watoto wadogo kooni. Karoti pia zinaweza kuwasakama watoto kooni!

A. R., Marekani

“Amkeni!” lajibu: Tunamshukuru msomaji huyu kwa maelezo yake. Gazeti moja linalohusu utunzaji wa watoto linasema hivi: “Ingawa watoto fulani wamewahi kusakamwa koo na kufa walipokuwa wakila vipande vya matofaa, karoti zisizopikwa, biskuti, na bisi, vyakula vinne ambavyo vimesababisha vifo vya watoto wengi zaidi ni soseji, njugu, peremende, na zabibu.” Hata hivyo, watunzaji wa afya wanawaonya wazazi kwamba karoti nzima-nzima zinaweza kuwa hatari kwa watoto wenye umri wa chini ya mwaka mmoja.

Uchapaji wa Biblia Asanteni kwa makala “Kimbilio la Wachapaji wa Biblia.” (Septemba 8, 2002) Siku hizi ni rahisi sana kupata Biblia katika lugha zetu hivi kwamba tunaweza kusahau jitihada za kujidhabihu za wale waliofanya jambo hilo liwezekane. Kusoma makala hiyo kulinifanya nimthamini Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo na utegemezo wake kwa kufanya Biblia ipatikane kwa watu wote wenye mioyo minyoofu.

E. S., Brazili

Kushuka Moyo Baada ya Kujifungua Imenibidi niwaandikie ili niwashukuru kwa ajili ya makala “Nilipambana na Ugonjwa wa Kushuka Moyo Baada ya Kujifungua.” (Julai 22, 2002) Mimi pia nilihuzunika baada ya kujifungua na nilihisi kabisa kama ambavyo mlitaja kwenye makala yenu. Niliona haya kuwaambia wengine jambo hilo. Hata nilihofia kwamba mume wangu hangenielewa. Kwa hiyo niliteseka tu, bila hata kufahamu tatizo langu. Ninamshukuru sana Yehova, na nyinyi pia, kwa msaada huo! Ingawa huenda nikashuka moyo mara kwa mara, nitaweza kuvumilia kwa urahisi zaidi.

F. L., Belarus

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 30]

Photo: Houston Chronicle