Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kwa Hakika Ninakipendekeza Kitabu Hicho”

“Kwa Hakika Ninakipendekeza Kitabu Hicho”

“Kwa Hakika Ninakipendekeza Kitabu Hicho”

Mwandishi maarufu wa Denmark, Erik Haaest, aliyenukuliwa hapa juu, alikuwa anazungumzia kitabu kipi?

Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu

Aliandika hivi: “Kuna miiko mingi nchini Denmark na nitavunja mwiko mmoja leo. Haifai kuwasifu Mashahidi wa Yehova kwa jambo lolote. Huo ndio mwiko ambao nitavunja.

“Kwa miaka mingi sana, wenzi wawili wa ndoa walio nadhifu wamekuwa wakinitembelea kila mwezi kuniletea gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Niliwaambia kitambo sana kwamba mimi sitaki kugeuzwa imani, lakini magazeti yao yana habari muhimu sana na yenye kupendeza—isipokuwa tu sehemu zenye mahubiri. Nimesoma makala nzuri sana katika magazeti hayo, na pia ni jambo lenye fahari kwamba nakala [milioni 21] za kila toleo huchapishwa.

“Hivi majuzi wenzi wale wa ndoa wenye kupendeza walinipatia kitabu [Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu], bila malipo yoyote. . . . Nilikisoma chote. Pia nilichunguza marejeo mengi kati ya yale ambayo yameonyeshwa, na kwa hakika ni mengi sana!

“Hiyo ndiyo historia ya dini yenye hoja sahihi na isiyopendelea dini yoyote ambayo nimewahi kusoma.

“Kwa hakika ninakipendekeza kitabu hicho. Ni kweli kinazungumzia pia imani ya Mashahidi wa Yehova, lakini hiyo ni sehemu ndogo sana ya historia hiyo bora ya dini.”

Ikiwa ungependa kupata kitabu hicho, tafadhali jaza kuponi iliyo hapa.

□ Ningependa kupokea kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Top left, Jewish man: Garo Nalbandian; top middle, Buddhist monk: G. Deichmann, Transglobe Agency, Hamburg