Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Barua Kutoka kwa Mpendwa

Barua Kutoka kwa Mpendwa

Barua Kutoka kwa Mpendwa

Msomaji mmoja kutoka New York alilinganisha kitabu Mkaribie Yehova na barua kutoka kwa mpendwa, akisema hivi: “Kila sura huchochea moyo na kuzidisha upendo wako kwa Yehova.” Akaongezea hivi: “Sasa nimemaliza kusoma kitabu chote, na nina hamu kubwa ya kuanza kukisoma tena, kama unavyoweza kusoma tena barua kutoka kwa mtu fulani unayempenda sana.” Ona maelezo ya watu wengine.

Msomaji mmoja huko Kansas alisema: “Nahisi kwamba ninaendelea kumkaribia zaidi Baba yangu wa mbinguni. Moyo wangu umejaa upendo . . . Ninatazamia sana kukisoma kila asubuhi, na nitakisoma tena na tena.”

Mwanamke mmoja kutoka Maine aliandika: “Kimenisaidia kumthamini Yehova zaidi! Maneno yaliyo katika ukurasa wa 74 yanafariji sana: ‘Kwa wale wanaokufa, hakuna mahali pengine salama pa kuwa isipokuwa katika kumbukumbu ya Mungu.’” Mwandishi mmoja huko Alaska akubaliana naye kwa kusema: “Kilinigusa moyo sana hivi kwamba nikalia machozi.” Aliongezea hivi: “Hakika nitakisoma tena na kukirudia tena na tena.”

Tunaamini kwamba utahisi vivyo hivyo ukisoma kitabu hicho. Baada ya sura tatu za kwanza, kitabu hicho kimegawanywa katika sehemu nne, “Hodari kwa Nguvu,” “Bwana Hupenda Haki,” “Mwenye Hekima Moyoni,” na “Mungu Ni Upendo.” Chamalizia kwa sura “Mkaribieni Mungu, Naye Atawakaribia.”

Unaweza kuomba kitabu hicho chenye kurasa 320 kilichojalidiwa kwa karatasi, kwa kujaza kuponi iliyo hapa chini na uitume kwa anwani iliyoonyeshwa hapa au kwa kutumia anwani iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea nakala ya kitabu Mkaribie Yehova.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo