Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Uhai Ulianzaje?

Uhai Ulianzaje?

Uhai Ulianzaje?

NCHINI Ufaransa, dhana ya mageuzi hufundishwa kuwa ukweli usiokanushika shuleni na katika vyombo vya habari. Hivyo, hata ikiwa watu wanamwamini Mungu, wao huona kwamba dhana ya mageuzi ndiyo inayoeleza chanzo cha uhai. Hata hivyo, watu wengi wanaovutiwa na utata wa viumbe wanaitilia shaka dhana hiyo. Ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Ufaransa ilipokea barua ifuatayo:

“Hivi majuzi nilipata kitabu chenu kinachoitwa Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? katika duka linalouza vitabu vilivyotumiwa. Kitabu hicho kidogo kilinipendeza sana, kwani ninaona kinazungumzia masuala muhimu. Kwa kuwa mimi ni mwanafizikia, kwa miaka mingi nimependezwa na maswali magumu yanayozushwa na ‘dhana ya Darwin’ na ‘dhana nyingine za mageuzi.’ Inadaiwa kwamba dhana hizo zinaeleza jinsi uhai ulivyotokana na vitu visivyo hai.”

Baada ya kusoma kitabu hicho ambacho alikiita “kitabu chenu kidogo,” mtu huyo alisema hivi: “Kitabu Life—How Did It Get Here? kimeandikwa vizuri sana na kinaeleza kwa ufupi matatizo na hoja zinazopingana ambazo zimesababishwa na dhana tata ya mageuzi ambayo inakubaliwa na wanasayansi wengi wa leo.” Kisha akaomba habari zaidi.

Ikiwa ungependa kupokea kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?, tafadhali jaza sehemu iliyo hapa chini na uitume ukitumia anwani iliyoonyeshwa au kwa kutumia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.