Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Michezo ya Kompyuta Nina umri wa miaka 13. Nilipoona gazeti lenye mfululizo wa makala wenye kichwa “Je, Michezo ya Kompyuta Ina Ubaya Wowote?” nilipendezwa sana nalo. (Desemba 22, 2002) Nilikuwa mchezaji sugu wa mchezo fulani uliozungumziwa kwenye ukurasa wa 7. Ninawashukuru kwa kuchapisha makala hizo kwa sababu zilinisaidia nibadilike na kumpenda Yehova zaidi.

J. L., Marekani

Hivi karibuni, nitafikisha umri wa miaka 15. Shuleni tuliambiwa tuandike insha kuhusu jambo lolote lililotukia hivi karibuni. Gazeti hilo la Amkeni! lilikuja kwa wakati unaofaa. Insha yangu ilipendwa sana darasani. Nilipata maksi nyingi pia! Tafadhali endeleeni kuandika makala kama hizo.

J. A., Ujerumani

Nimekuwa nikitaka kuwashukuru kwa habari mnazoandika katika magazeti yenu, lakini niliposoma makala kuhusu michezo ya kompyuta niliamua nitaandika papo hapo. Mimi ni mama wa watoto wawili, mmoja mwenye umri wa miaka 11 na mwingine wa miaka 3. Kwa hiyo, habari hiyo ilinifaa sana. Ninaona waziwazi jinsi Muumba wetu anavyotupenda na kutulinda kupitia magazeti kama haya.

O. V., Marekani

Abrolhos Nina umri wa miaka 13. Nilifurahia kusoma makala yenye kichwa, “Abrolhos Inavutia Macho.” (Desemba 22, 2002) Sikuzote nimependezwa na ndege wanaostaajabisha, lakini ninapendezwa hasa na mambo yanayotukia kwenye sakafu ya bahari na visiwani. Natumaini kwamba mtaendelea kuchapisha makala kama hizo.

V. J., Serbia na Montenegro

Nilifurahia kusoma makala hiyo. Iliandikwa kwa njia iliyonisaidia kuwazia nyangumi wakiruka juu ya maji, ndege maridadi wakiruka juu ya bahari, na matumbawe yenye samaki wa aina mbalimbali wanaolishwa na wanadamu. Ninavutiwa sana na Muumba, na ningependa kutembelea sehemu hiyo maridadi ya ulimwengu. Kwa sasa, nitatumia makala hiyo ninapozungumza na watu wanaodhani kwamba kuishi milele duniani hakuwezi kufurahisha.

M. P., Poland

Imani Yajaribiwa Nilifurahia makala yenye kichwa, “Imani Yajaribiwa Huko Slovakia.” (Desemba 22, 2002) Mara nilipomaliza kuisoma, nilianza kuandika barua hii. Sisi pia tunapaswa kubaki waaminifu kama vile Ján Bali alivyovumilia majaribu hayo. Sehemu yenye kupendeza zaidi katika makala hiyo ni jinsi alivyokumbuka maelezo mazuri kuhusu paradiso katika kitabu The Way to Paradise kilichochapishwa mwaka wa 1924. Nilifurahia sehemu hiyo kwa sababu inazungumzia ulimwengu mpya. Nina umri wa miaka tisa.

E. K., Hungaria

Uvutano wa Marika Tukiwa familia tumekuwa tukitaka kuwaandikia ili tuwashukuru kwa magazeti yenu mazuri. Hatimaye tuliamua kufanya hivyo baada ya kusoma makala yenye kichwa “Vijana Huuliza . . . Nawezaje Kuepuka Kuathiriwa na Vijana Wenzangu?” (Desemba 22, 2002) Makala hiyo ilitusaidia kufahamu jinsi kijana Daudi alivyomjua Yehova vizuri sana na jinsi alivyomtumaini sana. Daudi alifanikiwa kwa sababu hakutegemea maoni yake au yale ya wanadamu wengine. Ama kweli, ikiwa Yehova yu upande wetu, ya nini tuwaogope wanadamu wenzetu?

F H., Estonia

Nimekuwa nikisoma Amkeni! kwa miaka miwili, na sijawahi kuguswa hisia na kutiwa moyo sana kama niliposoma makala hiyo. Nilihisi kwamba iliandikwa kwa ajili yangu. Asanteni sana kwa habari hiyo inayonifaa.

T. C., Marekani