Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Insha Yake Ilivutia Kwelikweli

Insha Yake Ilivutia Kwelikweli

Insha Yake Ilivutia Kwelikweli

Alipokuwa katika mwaka wake wa mwisho, Ginny, mmoja wa Mashahidi wa Yehova huko Marekani, alipata fursa nzuri ya kuzungumza kuhusu dini yake. “Mwalimu alituambia kwamba tulihitaji kuandika insha ya mwisho ili tuhitimu,” akasema. “Nilimwambia kwamba ningependa kuandika kuhusu Mashahidi wa Yehova katika kambi za mateso za Nazi.”

Mwalimu alimpa Ginny ruhusa ya kuandika juu ya kichwa hicho. “Nilikuwa na wasiwasi wakati ulipofika wa kuwasilisha insha yangu na kuhutubia darasa,” akiri Ginny. “Sikujua kile ambacho wanafunzi wenzangu wangesema au kama wangenidhihaki.”

Ginny alianza hotuba yake kwa kuuliza hivi: “Je, kuna mtu yeyote anayejua ni nani waliovalia Nyota ya Daudi katika kambi za mateso za Nazi?” Kila mtu akajibu, “Ni Wayahudi.” Kisha akauliza kama kuna yeyote aliyejua ni nani waliovalia pembetatu ya zambarau. Hakuna aliyejibu. “Nikawaambia ni Mashahidi wa Yehova,” asema Ginny.

Mwalimu na wanafunzi walivutiwa sana na habari za Ginny. “Walistaajabu sana kujua kwamba Mashahidi wa Yehova wangeweza kuachiliwa kwa kutia tu sahihi kikaratasi fulani ili kukana imani yao,” asema Ginny. “Baadhi ya wanafunzi wenzangu waliniambia baadaye kwamba awali walikuwa wakiwadhihaki Mashahidi wa Yehova lakini wakati ujao watawasikiliza wakiwatembelea nyumbani kwao.”

Ginny alipata alama nne za A kwa ajili ya ripoti yake na hotuba yake. “Sikupata alama nzuri tu,” asema, “bali pia nilipata fursa nzuri ya kuongea kuhusu imani yangu!”

[Picha katika ukurasa wa 19]

Mashahidi wengi wa Yehova walipewa fursa ya kuachiliwa maadamu tu wangetia sahihi hati hii ya kukana imani yao

[Hisani]

Courtesy of United States Holocaust Memorial Museum