Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Fuliza Kufanya Lililo Jema”

“Fuliza Kufanya Lililo Jema”

“Fuliza Kufanya Lililo Jema”

“Ningependa kuwafahamisha kwamba jitihada na kazi yenu imetambuliwa na watu wanaojali usafi na pia maoni ya wageni kuhusu Mji wetu. Majengo yenu yanaonyesha jinsi mnavyopendezwa na mazingira mazuri na Mji wenyewe.”

Maneno hayo yalisemwa na meya wa mji wa Halton Hills, ambako ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Kanada imejengwa. Baadaye, meya huyo alitoa zawadi yenye maandishi kwa ofisi ya tawi, akitoa “shukrani kwa jitihada na kazi iliyofanywa ili kuboresha maisha ya wakazi wote wa Halton Hills.”

Shukrani kama hizo kutoka kwa wakuu wa serikali huonyesha ukweli wa andiko la Waroma 13:3, linalosema hivi: “Fuliza kufanya lililo jema, nawe utakuwa na sifa kutoka kwayo.” Hata hivyo, sifa na heshima zinapaswa kumwendea Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu mzima, Yehova.