Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kila Mtu Anapaswa Akisome”

“Kila Mtu Anapaswa Akisome”

Kila Mtu Anapaswa Akisome”

Hivyo ndivyo msomaji mmoja kutoka California, Marekani, alivyosema kuhusu kitabu Mkaribie Yehova. “Kina ujumbe mzuri, picha maridadi, na kina thamani kubwa ya kiroho,” alisema. Halafu akaongezea hivi: “Asanteni sana kwa kitabu hicho cha ajabu kumhusu Mungu wetu mkuu.”

Wengine wametoa maelezo kama hayo pia, kama mifano hii inavyoonyesha: “Sasa kwa kuwa nimemaliza kukisoma chote, kwa kweli nimehuzunika kidogo kwa kuwa nimekimaliza. Lakini nina hamu ya kukisoma tena—mara hii kwa uangalifu, nikitafakari kwa uzito mambo yaliyomo.”

Mwingine aliandika hivi: “Habari inayohusu huruma ya Mungu na jinsi alivyo tayari kusamehe ilinigusa moyo sana na kunifanya nihisi kuwa karibu na Baba yetu wa mbinguni na Mpaji wa Uhai.”

Tuna hakika kwamba kwa kukisoma utamkaribia zaidi Baba yetu wa mbinguni, Yehova. Kimegawanywa katika sehemu nne yaani, “Hodari kwa Nguvu,” “Bwana Hupenda Haki,” “Mwenye Hekima Moyoni,” na “Mungu Ni Upendo.” Sura tatu za kwanza zinatanguliza sehemu hizo ambazo zinakazia sifa kuu za Mungu. Sura ya 31 ambayo ni ya mwisho ina kichwa “Mkaribieni Mungu, Naye Atawakaribia.”

Unaweza kuomba kitabu hicho chenye jalada nyepesi kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Naomba kitabu Mkaribie Yehova.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.