Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Faragha Nilivutiwa na kichwa “Je, Faragha Yako Inaingiliwa?” (Januari 22, 2003) kwa kuwa mimi ni mwandishi wa kitabu kimoja kinachozungumzia habari hiyo ambacho hununuliwa sana. Mwandishi wenu alifanya kazi nzuri sana. Nina dokezo lingine: Ukiombwa ujitambulishe, afadhali utoe pasipoti kwani haina anwani wala nambari ya akaunti yako ya malipo ya uzeeni.

J. L., Hispania

Vitu Maridadi Asanteni kwa makala “Vitu Maridadi Kutoka Ufuoni.” (Januari 22, 2003) Kama mwandishi wa makala hiyo, tulifurahi sana tulipokusanya makombe ya konokono na moluska. Tunafurahia sana kukusanya makombe ufuoni. Kila tunapotazama makombe hayo tunashangazwa na usanii wenye hekima wa Muumba.

W. na M. P., Ujerumani

Tangu nilipokuwa na umri wa miaka 12 hivi, nilipendezwa na makombe. Baada ya kuyakusanya kwa miaka 20, nilihisi nimekusanya ya kutosha. Lakini niliposoma makala hiyo na kujifunza kwamba kuna aina 50,000 hivi za moluska, nilishangaa kutambua kwamba nilikuwa nimekusanya makombe machache sana na nilistaajabishwa hata zaidi na uumbaji wa Yehova.

M. S., Paraguay

Meli za Matete Nilipendezwa sana na makala yenye kichwa “Kusafiri Baharini kwa Meli ya Matete!” (Januari 22, 2003) Katika usomaji wangu wa Biblia, nilisoma andiko la Ayubu 9:26, Biblia Habari Njema. Likieleza ufupi wa maisha ya wanadamu, andiko hilo linasema hivi: ‘Yapita kasi kama mashua ya matete.’ Mimi na rafiki yangu mmoja tulishangaa ni kwa nini Ayubu alilinganisha maisha mafupi na mashua ya matete. Rafiki yangu alisema kwamba huenda Ayubu alimaanisha kwamba “matete hulowa pole kwa pole” na kuharibika, kama makala hiyo inavyosema.

N. D., Marekani

“Amkeni!” linajibu: Kulingana na kitabu kimoja cha marejeo, Ayubu alikuwa anasema kuhusu mwendo wa kasi wa meli hizo nyepesi. Iwapo hiyo ni kweli, maana ni ileile, kwamba maisha ya mwanadamu ni mafupi.

Flamingo Tulipofungua toleo hilo la Amkeni!, mimi na mume wangu tuliona makala “Ndege Wenye Rangi ya Waridi.” (Januari 22, 2003) Mume wangu alisema hivi: “Hii inakufaa.” Anajua jinsi ninavyopenda uumbaji wa Yehova na hasa flamingo mwenye kupendeza wa rangi ya waridi. Natamani kuwaona ndege hao kwa macho yangu. Asanteni sana kwa makala hiyo. Ilinifunza mengi.

M. N., Jamhuri ya Cheki

Kuiba Mtihani Nina umri wa miaka 11. Nilifurahia makala “Vijana Huuliza . . . Kuna Ubaya Gani Kuiba Mtihani? (Januari 22, 2003) Hata ingawa huwa sifaulu sana katika mitihani, ninajua kwamba alama ninazopata ni zile ambazo nimefanyia kazi. Ama kweli, baadhi ya wanafunzi wenzangu ambao huiba mitihani hupata alama chache kuliko mimi! Isitoshe, dhamiri yangu ni safi na hilo ndilo jambo la maana zaidi.

Z. T., Austria

Nina zoea la kuiba mitihani, labda kwa sababu sikuliona kuwa jambo zito. Makala hiyo itanisaidia nikumbuke maandiko kama vile Waebrania 13:18, ambayo yatanisaidia wakati ninaposhawishiwa kuiba mitihani wakati ujao.

N. I., Italia

Niko katika kidato cha pili. Wakati mwingine nilijaribu kuiba mitihani, bila kutambua kwamba huko ni kuiba! Lakini makala hiyo imenifanya niazimie kuwa na dhamiri safi.

K. G., Estonia