Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Mwaka wa Biblia”

“Mwaka wa Biblia”

Mwaka wa Biblia”

Mwaka wa 2003 umetajwa kuwa “Mwaka wa Biblia” nchini Austria, Ufaransa, Ujerumani, na Uswisi. Gazeti la Ujerumani Frankfurter Allgemeine Zeitung linasema hivi: “Mwaka wa Biblia ulisherehekewa kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 1992, na kama ilivyokuwa wakati huo pia, [makanisa] yanataka kuwaelimisha watu kuhusu ‘kitabu hicho cha uhai’ na kuonyesha thamani ya kitamaduni ya Maandiko hayo Matakatifu.”

Kulingana na gazeti Bibelreport la Juni 2002, Biblia nzima au sehemu yake, imetafsiriwa katika lugha 2,287. Pia inakadiriwa kwamba kufikia sasa, Biblia bilioni 5 hivi zimegawanywa. Jitihada zote hizo zinaonyesha wazi kwamba watu wanakiheshimu kitabu hicho.

Huenda watu wengi leo hawaamini kwamba Biblia ina faida yoyote. Ama kweli, wengi wanaona kwamba kanuni za Biblia ni za kale na hazipatani na maisha ya kisasa. Hata hivyo, makanisa nchini Ujerumani yanatazamia kutimiza mambo mawili katika Mwaka huu wa Biblia—kuwatia watu moyo waishi kupatana na kanuni za Biblia na kuwachochea wale ambao hawaendi kanisani wapendezwe na Biblia.

Kuisoma Biblia nzima si jambo rahisi, lakini hiyo ndiyo njia nzuri ya kujua mambo makuu yaliyomo katika Maandiko. Hata hivyo, mtu anayetaka kufaidika kutokana na Biblia anahitaji kufikiria maneno ya 2 Timotheo 3:16, 17: “Andiko lote limepuliziwa na Mungu na ni lenye manufaa kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu apate kuwa hodari, aliyeandaliwa vifaa kikamili kwa ajili ya kila kazi njema.”

Mshairi Mjerumani Johann Wolfgang von Goethe (1749-1832) alisema hivi: “Ninaamini kwamba Biblia hupendeza zaidi kadiri mtu anavyoielewa.” Ama kwa hakika, Neno la Mungu pekee ndilo linaloeleza vizuri tunakotoka, kwa nini tunaishi, na kuhusu wakati ujao!—Isaya 46:9, 10.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]

From the book Bildersaal deutscher Geschichte