Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Siri ya Kuwa na Ndoa Yenye Mafanikio

Siri ya Kuwa na Ndoa Yenye Mafanikio

Siri ya Kuwa na Ndoa Yenye Mafanikio

“Kudanganya kidogo ndiyo siri ya kuwa na uhusiano mzuri wa kimapenzi,” lasema gazeti La Presse. Gazeti hilo la Kanada lilikuwa likiripoti kuhusu uchunguzi ulioonyesha kwamba uwongo unafaa. Uchunguzi huo ulichapishwa katika gazeti Journal of Social and Personal Relationships. Profesa Tim Cole wa Chuo Kikuu cha De Paul, Chicago, Marekani, anasema hivi: “Tunaweza kudumisha uhusiano [wa kimapenzi] kwa kudanganya [au kusema uwongo] kidogo tu bila kuuhatarisha.”

Lakini je, kweli kudanganya ndiyo siri ya kuwa na ndoa yenye mafanikio? Biblia inawahimiza Wakristo hivi: “Sasa kwa kuwa mmeweka mbali ukosefu wa lililo kweli [uwongo], semeni kweli kila mmoja wenu pamoja na jirani yake.” (Waefeso 4:25) Je, shauri hilo lina matokeo? Wakili mmoja wa talaka alipoulizwa, Ni nini kisababishi kikuu cha talaka? alijibu hivi: “Kushindwa kuzungumza pamoja kwa unyoofu, kutofunua yaliyo moyoni na kutotendeana kama marafiki wakubwa zaidi.”

Basi siri ya kuwa na ndoa yenye furaha ni nini? Sura ya 3 ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia ina kichwa “Funguo Mbili za Kuwa na Ndoa Yenye Kudumu.” Sura hiyo inazungumzia mambo mawili muhimu yanayofanya wenzi wa ndoa waishi kwa furaha na kupata baraka nyingi. Unaweza kuomba kitabu hiki kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Naomba kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.