Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Wanawake Wanastahili Staha”

“Wanawake Wanastahili Staha”

“Wanawake Wanastahili Staha”

Mwanafunzi wa chuo mwenye umri wa miaka 17 huko India alishiriki katika mashindano ya kuongea mbele ya watu yaliyopangwa na shule yao. Aliamua kutumia Amkeni! la Desemba 8, 1992, lenye makala “Wanawake Wanastahili Staha.”

Kichwa cha habari yake kilikuwa “Wanawake—Je! Wanastahiwa Leo?” Matokeo yakawa nini? Anasema hivi: “Nilishinda zawadi ya kwanza katika mashindano hayo.” Kisha aongezea hivi: “Ningependa kuwashukuru sana kwa ajili ya Amkeni! Linatusaidia sana sisi vijana kwa sababu linatuelimisha na kutuarifu habari za karibuni. Pia linatusaidia kukabiliana na magumu ya ulimwengu huu.”

Je, umefurahia kusoma toleo hili la Amkeni!? Gazeti hili huandikwa ili kuelimisha familia nzima, si vijana tu. Huchunguza sana matukio ya sasa na hueleza maana ya kweli ya matukio hayo. Huchapishwa mara mbili kwa mwezi katika Kiswahili. Usikose toleo lolote!