Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Faraja kwa Wakati Unaofaa

Faraja kwa Wakati Unaofaa

Faraja kwa Wakati Unaofaa

Watu wengi wanahitaji faraja katika siku hizi za hatari, hasa wanapofiwa na wapendwa wao. Mwanamke mmoja alifiwa na mama yake na mimba yake ikaharibika muda mfupi baadaye. Aliiandikia hivi ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Mexico: “Nilifarijika sana nilipopata broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Ina habari muhimu na ilinifaa sana. Asanteni kwa upendo wenu wa Kikristo na bidii yenu ya kuchapisha vitabu vya Biblia kama broshua hiyo.”

Alifarijiwa hasa na maandiko ambayo yamenukuliwa katika broshua hiyo. Kwa mfano, 1 Wakorintho 15:26 linasema: “Kikiwa ni adui wa mwisho, kifo kitafanywa kuwa si kitu.” Huenda wewe au mtu unayemjua atafarijika akisoma broshua hiyo yenye kurasa 32. Broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa huzungumzia vichwa kama vile “Ninaweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?,” “Wengine Waweza Kusaidiaje?,” na “Tumaini Hakika kwa Wafu.”

Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Naomba broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.