Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jina la Mungu Kwenye Jumba la Kifalme

Jina la Mungu Kwenye Jumba la Kifalme

Jina la Mungu Kwenye Jumba la Kifalme

NA MWANDISHI WA AMKENI! NCHINI SLOVAKIA

SLOVAKIA ni nchi ndogo yenye kupendeza sana katikati ya Ulaya. Eneo lake la mashambani lenye kuvutia lina majumba mengi ya kifalme yanayoonyesha utajiri na historia ndefu ya eneo hilo. Mojawapo ya majengo yenye kuvutia ni Jumba la Kifalme la Orava, lililojengwa juu ya majabali ya chokaa yenye urefu wa meta 112 yaliyo karibu na kijiji.

Maandishi ya kwanza kuhusu Jumba la Kifalme la Orava ni ya mwaka wa 1267. Tangu wakati huo limemilikiwa na watu mbalimbali. Mnamo mwaka wa 1556, jumba hilo lilimilikiwa na familia tajiri ya Thurzó. Familia hiyo ilirekebisha na kupanua jengo hilo na pia ilijenga kanisa dogo.

Kila mwaka makumi ya maelfu ya wageni kutoka nchi nyingi huja kuona Jumba la Kifalme la Orava na vivutio vingine. Katika ua, wageni wanaweza kuona jambo la kupendeza kwenye mchongo wa nembo ya familia ya Thurzó uliotengenezwa kwa jiwe-mchanga. Mchongo huo unaonyesha jina la Mungu lililo katika Biblia, Yehova, katika Kilatini.