Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Walifahamu Kwamba Mungu Anawapenda

Walifahamu Kwamba Mungu Anawapenda

Walifahamu Kwamba Mungu Anawapenda

Watu wengine wanafikiri kwamba hawapendwi kikweli na mtu yeyote—hata Mungu. Kwa hiyo, baada ya kusoma kitabu Mkaribie Yehova, wengi waliandika barua kutoa shukrani kwa uhakikisho ambao kinatoa. Mwanamke mmoja kutoka Decatur, Illinois, Marekani, aliandika hivi: “Nachachawa kufahamu kwamba Mungu ananipenda sana, hata nikiwa na kasoro nyingi.”

Alisema hivi pia: “Nilitoa machozi ya furaha niliposoma taarifa hii [kwenye ukurasa wa 117]: ‘Akiwa Baba mwadilifu au mwenye haki, Yehova ni thabiti kwa mambo yaliyo sawa na vilevile huwaonyesha rehema nyororo watoto wake wa kidunia ambao wanahitaji msaada na msamaha wake.’”

Mwanamume mmoja huko Ripon, California, aliandika hivi: “Asanteni sana kwa kunifahamisha kwamba Yehova ananipenda na kunijali. Ananithamini.” Mwanamke mmoja huko New Hampshire alisema: “Nyakati nyingine sitaki kuacha kusoma kitabu hicho.” Alieleza hivi: “Haikuwa rahisi kwangu kuamini kwamba Yehova anaweza kunipenda.” Kwa hiyo, kitabu hicho kilifika kwa wakati unaofaa.

Tuna hakika utafaidika pia kwa kusoma kitabu hicho. Baada ya sura tatu za kwanza, kuna sehemu nne zenye vichwa “Hodari kwa Nguvu,” “Bwana Hupenda Haki,” “Mwenye Hekima Moyoni,” na “Mungu Ni Upendo.” Kila sehemu inazungumzia sifa moja kuu ya Mungu. Sura ya mwisho ya kitabu hicho chenye kutia moyo ina kichwa “Mkaribieni Mungu, Naye Atawakaribia.”

Unaweza kuomba kitabu hicho cha kurasa 320 chenye jalada nyepesi kwa kujaza sehemu iliyo hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kupokea kitabu Mkaribie Yehova bila malipo.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.